Magazeti mbalimbali yaliandika juu ya ajali ya treni ya abiria ya reli ya kati iliyoua zaidi ya watu 100 (mia moja). Treni hiyo ilikua ikitokea jijini Dar es Salaam kwenda Mwanza na Kigoma na kupata ajali kati ya kijiji cha Igenndu na Msagali, Dodoma saa 5:00 asubuhi baada ya kurudi nyuma na kugongana na treni ya mizigo baada ya kushindwa kupanda kilima.