Usawiri wa wahusika wanawake katika ngano za kinyiramba

Date

2012

Journal Title

Journal ISSN

Volume Title

Publisher

University of Dar es Salaam,

Abstract

Lengo la utafiti huu lilikuwa ni kuchunguza usawiri wa wa ngano za husika wanawake katika Kinyiramba. Lengo hili limeweza kufanikiwa kutokana na kukamilika kwa malengo mahususi yaliyohusu kuchunguza dhamira mbalimbali za usawiri wa rnwanamke katika ngano, kubainisha na kuchambua usawiri wa wahusika wanawake katika ngano hizo. Maandiko na machapisho mbalimbali juu ya ngano na nafasi ya mwanamke yamepitiwa kwa kutumia nadharia. Uhalisa. Utafiti umetumia mbinu ya uchambuzi matinikatika kukusanya data za msingi za utafiti pamoja na data za upili kutoka maandiko mbalimbali. Uchambuzi wa data umeongozwa na mbinu ya uchambuzi wa kifasihi. Matokeo ya utafitiyanaonesha kwamba, wahusika wanawake wamesawiriwa kwa mtazamo hasi katika ngano hizi kuliko ule chanya. Aidha uchunguzi umegundua kwamba ngano hizi zimeyazungumzia masuala mbalimbali yanayowakandamiza wanawake katika jamii ikiwepo mfumo dume. Miongoni mwa masuala hayo ni uhuru wa mwanamke ambao hujengwa na dhamira nyingine kama vile ulezi, uzalishaji mall, uvurnilivu, ushujaa, umalaya, uchawi, rnwenye wive, chombo cha starehe na kadhalika. Utafiti umegundua kwamba hit imetokana na mfumo wa jamii unavyomtazama mwanamke. Mwisho limetolewa hitimisho kuu la utafiti, lililoainisha nyanja mbalimbali za kiutafiti zinazoweza kuibuliwa katika wahusika wengine katika kazi za fasihi simulizi hususani ngano.

Description

Available in print form, East Africana Collection, Dr. Wilbert Chagula Library, Class mark ( THS EAF PL 8025.T34K578 )

Keywords

Nyiramba (African people), Women participation

Citation

Kitundu, N J (2012) Usawiri wa wahusika wanawake katika ngano za kinyiramba, Master dissertation, University of Dar es Salaam. Dar es Salaam