Dhamira za nyimbo za harusi za wakerewe na mabadiliko ya jamii

Date

2012

Journal Title

Journal ISSN

Volume Title

Publisher

University of Dar es Salaam,

Abstract

Tasinifu hii ni matokeo ya utafiti kuhusu Dhamira za Nyimbo za Harusi za Wakerewe na Mabadiliko ya Jamii. Utafiti ulikusudia kuchunguza mabadiliko ya jamii ya Wakerewe jinsi yanavyoakisiwa na dhamira za nyimbo za harusi za Wakerewe. Nyimbo kumi zilizoimbwa kuanzia miaka ya 1970 hadi mwaka 2010 ndizo zilizochungunzwa katika utafiti huu. Nyimbo hizo zimekusanywa kutoka vijiji vya Bukindo na Buzegwe katika wilaya ya Ukerewe.Nyimbo za harusi kumi zilizokusanywa zilichambuliwa ili kuweza kubainisha mabadiliko ya jamii yanavyoakisiwa na dhamira katika jamii ya Wakerewe. Aidha, nadharia ya Sosholojia ilitumika katika uchambuzi wa data. Njia za ushuhudiaji na mahojiano zilisaidia kupata data katika kutimiza lengo la kuchunguza dhamira na mabadiliko ya jamii. Utafiti wetu ulibaini kuwa nyimbo za harusi za Wakerewe huakisi mabadiliko yanayojitokeza katika jamii. Mabadiliko yaliyoakisiwa katika dhamira nyimbo hizo ni pamoja na maendeleo ya sayansi na teknolojia, kuingia kwa ugonjwa wa UKIMWI na kuibuka kwa imani za ushirikina kuhusu maalbino.Mapendekezo ya utafiti huu yalitolewa kwa watafitiwa kufanya tafiti nyingi zaidi katika fani na maudhui kwenye nyimbo za harusi za jamii mbalimbali nchini

Description

Available in print form, East Africana Collection, Dr. Wilbert Chagula Library, Class mark (THS EAF PL8025.T34M83)

Keywords

Kerewe language, Kerewe (African people), Wedding songs, Bantu languages

Citation

Mugassa, A H F (2012) Dhamira za nyimbo za harusi za wakerewe na mabadiliko ya jamii, Tasnifu ya Uzamili, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam