Makosa ya kiisimu katika uandishi wa magazeti
Date
Authors
Journal Title
Journal ISSN
Volume Title
Publisher
Abstract
Utafiti huu unashughulikia makosa ya kiisima katika Uandishi wa magazeti hususani magazeti ya Kiswahili ya uhuru wa mtanzania ya nchini Tanzania ya kuanzia Julai hadi Disemba, 2010. Malengo ya utafiti huu ni kubainisha na kuainisha makosa yanayojitokeza katika uandishi wa magazeti, kuelezea sababu za ujitokezaji wa makosa hayo pamoja pamoja na kupendekeza mbinu za kuyapunguza au kuyakomesha kabisa. Ili kufikia lengo hilo, utafiti huu ni nadharia ya Isimu zalishi (Geerative Linguistic Theory) na hasa mkabala wa umilisi na utumizi wa kiisimu (Linguistic competence and Perfomance) ambayo hushughulikia usahihi wa lugha katika matawi yote ya isimu ambayo ni fonolojia, mofolojia, sintaksia na semantic. Vyanzo vya makosa hayo vimebainika kuwa ni pamoja na kutokuelewa maana za maneno yanayotumika katika uandishi, athari za lugha ya mazungumzo katika uandishi pamoja na mazoea mabaya ya matumizi ya maneno mbalimbali. Aidha baadhhi ya mapendekezo yaliyotolewa ili kukomesha kama si kupunguza kabisa utokeaji wa makosa hayo ni pamoja hayo ni pamoja na kuboresha mfumo mzima wa ufundishaji na kuwajengea stadi stahiki za lugha za uandishi makini