Repository logo
  • English
  • Català
  • Čeština
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • Latviešu
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Log In
    New user? Click here to register. Have you forgotten your password?
Repository logo
    Communities & Collections
    All of DSpace
  • English
  • Català
  • Čeština
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • Latviešu
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Log In
    New user? Click here to register. Have you forgotten your password?
  1. Home
  2. Browse by Author

Browsing by Author "Sosoo, Felix Kwame"

Now showing 1 - 2 of 2
Results Per Page
Sort Options
  • No Thumbnail Available
    Item
    Ulinganishi wa mwanamke mwanamapinduzi katika tamthilia za kiswahili za nguzo mama (1982) na ngoma ya ng’wanamalundi (1988)
    (University of Dar es Salaam, 2014) Sosoo, Felix Kwame
    Lengo kuu la utafiti huu lilikuwa kuchunguza nafasi ya mwanamke mwanamapinduzi katika tamthilia za Nguzo Mama (1982) na Ngoma ya Ng’wanamanalundi (1988). Malengo mahususi yalikuwa matatu nayo ni kuchunguza jinsi waandishi wa tamthilia za Nguzo Mama (1982) na Ngoma ya Ng’wanamalundi (1988) walivyomsawiri mwanamke mwanamapinduzi; kubainisha tofauti zinazojitokeza kumhusu mhusika mwanamke mwanamapinduzi kati ya waandishi wawili tofauti na pia kuainisha sababu za kijamii na kiujumi zinazowafanya waandishi wa kazi teule kumsawiri mwanamke mwanamapinduzi kwa jinsi walivyomsawiri. Nadharia ya Ufeministi hasa wa Afrika ndiyo iliyotumika katika uchambuzi wa data ya tasnifu hii. Mbinu za ukusanyaji wa data maktabani kwa kusoma maandiko na machapisho mbalimbali kwenye magazeti, majarida, vitabu vinavyohusu mada husika, makala na pia mtandao ndizo zilizotumika katika utafiti huu. Tasnifu mbalimbali za mwanzo zilizozumgumzia usawiri wa mwanamke kwa namna mbalimbali pia zilitumika kupata taarifa, hasa kuhusu mwanamke. Matokeo ya utafiti yanaonesha kwamba waandishi wamemsawiri mwanamke kama mwanamapinduzi wa kifikra na kiitikadi kupitia elimu, matabaka, utamaduni na haki za wanawake na watoto. Vilevile utafiti huu umebaini kwamba ingawa waandishi wote wanatumia dhamira zinazofanana, wanatofautiana katika usawiri wa wahusika hasa mitazamo yao kuhusu nani anayestahili kuleta maendeleo ya kweli katika jamii. Mbogo ambaye ni mwandishi mwanaume (1988) anamsawiri mwanamke kama mwanamapinduzi lakini katika hali ya kumbeza; tofauti na Muhando (1982) ambaye ni mwandishi mwanamke, anamsawiri mwanamke mwanamapinduzi kama mdadisi wa mambo ambaye safari yake ya ukombozi inaanza kwa mchakato wa kujifunza kutokana na ugumu wa maisha anayopitia katika mfumo dume. Hali kadhalika, utafiti huu umebaini kwamba Mbogo anatumia mfumo dume kama sababu za kijamii katika kumsawiri mwanamke mwanamapinduzi. Katika kufanya hivi, anamchora mwanamume kuwa mtu wa kwanza kupata utambuzi na baadaye kumjuza mwanamke. Hii ni tofauti na Muhando ambaye anaonekana kujaribu kuupinga mfumo dume na kusawiri usawa wa kijinsia, akionesha kuwa hakuna mfumo bora kuliko mwingine. Anasisitiza kuanzishwa kwa usawa wa kijinsi na kijinsia.
  • Loading...
    Thumbnail Image
    Item
    Ushujaa katika motifu ya safari ya msako: ulinganishi wa ngano za kiewe kutoka ghana na riwaya za Shaaban robert kutoka Tanzania.
    (University of Dar es Salaam, 2018) Sosoo, Felix Kwame
    Utafiti huu ulihusu ushujaa katika motifu ya safari ya msako ulinganishi ukiwa katika ngano za Kiewe kutoka Ghana na riwaya teule za Shaaban Robert kutoka Tanzania. Tulifanya utafiti kutokana na mgongano wa kinadharia ambapo kuna wataalamu wa fasihi wanaoona kuwa, kwa vile kila jamii ina utamaduni wake, kazi zao za fasihi hutofautiana na wengine wanaoona kuwa jamii zenye mfanano mkubwa wa kiutamaduni huweza kuwa na kazi za fasihi zinazofanana. Lengo kuu la utafiti huu ni kuchunguza na kulinganisha ushujaa unaosawiriwa katika motifu ya safari ya msako kwenye ngano za Kiewe na riwaya teule za Shaaban Robert. Aidha, utafiti huu ulikuwa na malengo mahususi manne ambayo ni: Kubainisha ushujaa unaosawiriwa katika motifu ya safari ya msako katika ngano za Kiewe na riwaya teule za Shaaban Robert; kueleza kufanana na kutofautiana kwa ushujaa unaosawiriwa katika motifu ya safari ya msako kwenye ngano za Kiewe na riwaya teule za Shaaban Robert; kufafanua jinsi ushujaa unaosawiriwa katika motifu ya safari ya msako unavyobainisha utamaduni na falsafa ya Kiafrika katika ngano za Kiewe na riwaya teule za Shaaban Robert; na kubainisha dhima ya ushujaa unaosawiriwa katika motifu ya safari ya msako kwenye ngano za Kiewe na riwaza teule za Shaaban Robert katika maendeleo ya fasihi. Ili kuweza kutimiza malengo hayo, data zilikusanywa kwa kutumia mbinu za aina mbili, ambazo ni majadiliano/mahojiano ya vikundi na udurusu matini. Mkabala wa uchambuzi uliotumika ni ule wa kitaamuli. Aidha, uchambuzi huo ulifanywa kwa kutumia ruwaza ya shujaa, nadharia ya Ontolojia ya Kiafrika na nadharia ya Mwingilianomatini. Kuhusu matokeo ya utafiti, imebainika kuwa ngano za Kiewe na riwaya teule kwa kiasi kikubwa zimesheheni ushujaa unaosawiriwa katika motifu ya safari ya msako. Aidha, imebainika kuwa, kuna mfanano mkubwa baina ya ushujaa unaosawiriwa katika motifu ya safari ya msako katika ngano za Kiewe na riwaya teule. Pia, utafiti huu umebaini kuwa ushujaa unaosawiriwa katika motifu ya safari ya msako katika tanzu husika unabainisha utamaduni na falsafa ya Kiafrika. Mwisho, utafiti huu umebainisha dhima ya ushujaa unaosawiriwa katika motifu ya safari ya msako kwenye ngano za Kiewe na riwaza teule za Shaaban Robert katika maendeleo ya fasihi teule. Mbali na kufafanua masuala hayo, bado utafiti wa kina unahitajika katika maeneo mbalimbali. Kwanza, kuna haja ya kufanya utafiti utakaohusisha ngano nyingi zaidi na riwaya nyingine zaidi ya zilizotumika katika utafiti huu. Pia, utafiti zaidi utakaohusisha tanzu nyingi zaidi unahitajika ili kutoa mahitimisho ya kimajumui.

About Library

The University of Dar es Salaam Library is a vital source of scholarly information that facilitates users to get access to learning and research resources during their studies. It provides access to a wide range of resources in both print and digital formats and conducive reading environment for users, regardless of their physical conditions. All registered users are eligible to access library resources and can borrow print materials from general shelves for a specific period of time.

Useful Links

Koha Staff Login

University Research Repository

WebMail

Aris

Book Study Room

Mara Oral History

Hansard

SOCIAL MEDIA

Instagram

Facebook

Twitter

YouTube

WhatsApp

Ask Librarian

Contact Us

Postal Address
P.O.Box 35092
Dar es Salaam

Call Us: +255 22 2410500/9 Ext. 2165 ; Direct line +255 22 2410241

Fax No:: +255 22 2410241

Email:: directorlibrary@udsm.ac.tz

2025 University of Dar es Salaam - University Of Dar Es Salaam Library
Term of use / Privacy Policy