Repository logo
  • English
  • Català
  • ÄŒeÅ¡tina
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • LatvieÅ¡u
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Log In
    New user? Click here to register. Have you forgotten your password?
Repository logo
    Communities & Collections
    All of DSpace
  • English
  • Català
  • ÄŒeÅ¡tina
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • LatvieÅ¡u
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Log In
    New user? Click here to register. Have you forgotten your password?
  1. Home
  2. Browse by Author

Browsing by Author "Charles, Asnath"

Now showing 1 - 2 of 2
Results Per Page
Sort Options
  • Loading...
    Thumbnail Image
    Item
    Fonolojia ya Kigweno.
    (University of Dar es Salaam, 2011) Charles, Asnath
    Utafiti huu umelenga kubainisha miundo ya silabi za Kigweno, michakato ya kifonolojia pamoja na athali zake katika konsonati na irabu za Kigweno. Katika utafiti huu tumetumia hojaji pamoja na kusikiliza mazungumzo ya wazawa kupata data ambapo watoa taarifa wasiopungua 60 kutoka vijiji vya Vuchama. Mangio, Mcheni na Mwaniko walishilikishwa. Nadharia iliyotuongoza Katika uchanganuzi wa data ni nadharia ya Umbo Upeo (UU) ambayo inaachana na matumizi ya kanuni na sheria na badala yake inatumia seti ya mashartizuizi ili kufikia upeo wa ukubalifu. Matokeo ya utafiti yanabainisha kuwa, kuna miundo minne ya silabi za Kigweno ambayo ni 1, K,KI na KKI. Tumebaini pia kuwa Kjgweno kina michakato kadhaa ya kifonolojia inayoathiri konsonanti na ile inayoathiri irabu. Inayoathiri irabu ni pamoja na Udondoshaji wa Irabu, Muungano wa irabu. Tangamano la irabu. Uchopekaji wa irabu, Unazalishaji wa irabu pamoja na kanuni ya Uyeyushali. Kwa upside wa michakato inayohusu konsonanti tumebaini kuwepo kwa usilimisho pamwe wa nazali.
  • Loading...
    Thumbnail Image
    Item
    Mvutano Kati Ya Maarifa Ya Kijaala Na Maarifa Ya Kijarabati Katika Maudhui Ya Filamu Za Kiswahili Nchini Tanzania
    (University of Dar es salaam, 2019) Charles, Asnath
    Tasnifu hii inahusu mvutano kati ya maarifa ya kijjaala na maarifa ya kijarabati katika maudhui ya filamu za Kiswahili nchini Tanzania. Malengo mahususi yalikua manne ambayo ni kubainisha vipashio vya sanaa vinavyodokeza udhihirikaji wa maarifa ya kijaala na maarifa ya kijarabati, kuchambua dhamira zinazodokeza mvutano kati ya maarifa ya kijaala na maarifa ya kijarabati , kueleza sababu za kuzuka kwa mvutano katika jamii ya kitanzania. Data za maktabani zilikusanywa kwa kutazama sidii na data za uwandani zilikusanywa kwa mbinu ya hoja za usahili .Utafiti huu umetumia mkabala wa kitaamuli na mkabala wa kitakwimu.Mkabala wa kitaamuli ulisaidia kuchanganua data kutoka katika utazamaji wa filamu na data kutoka kwa watunzi wa filamu teule kwa njia ya usaili.Mkabala wa kitakwimu ulitumika kuchanganua data za hojaji toka kwa watazamaji ambazo ziliwekwa katika program ya SPSS. Data za uwandani zilikusanywa katika mikoa miwili, dar es salaam na Arusha. Idadi ya filamu teule n inane.mbili kwa kila mtunzi.Filamu hizo ni Gods kingdom na revelation za Emmanuel Myamba,Mkwe na Big surprise za Lea Mwendamseke, White Maria na point of no return za Mtitu Game na Jini Sonia na Radi Kobra za July Tax. Utafiti huu umeongozwa na nadharia mbili, semiotiki na Mwitiko wa msomaji.Nadharia ya semiotiki ilitumika katika lengo la kwanza na la pili. Utafiti huu uligundua kuwa , filamu teule zina vipashio9vilivyorejelewa pia kama misimbo na ishara) vingi vinavyodokeza dhana hizi mbili.Misimbo hiyo ni pamoja na wahusika , msimbo wa kiishara, msimbo wa kimatendo na matukio pamoja na mandhari.Aidha , utafiti huu umebaini kuwa , filamu teule zimejaa dhamira zenye mvutano kati ya ujaala na ujarabati ambazo ni pamoja na nguvu ya uhai, vifo na wafu,ukatili na utu, masuala ya kiuchumi, vyanzo vya magonjwa na matibabu yake,uchawi na uganga pamoja na mapenzi na ndoa . Watunzi na watazamaji pia walithibitisha kuwapo kwa maudhui yenye mvutano huu katika filamu nyingine za Kiswahili. Nadharia ya mwitiko wa msomaji, ilitumika katika lengo la tatu na lengo namba nne . Sababu za mvutano zilizopatikana kwa watunzi na watazamaji ni pamoja na uhalisia wa jamii ya kitanzania,tofauti za kimazingira na nyakati, changamoto za kiutafiti kwa watunzi,kutofautiana kwa viwango vya elimu, kujitosheleza kwa ujaala na ujarabati pamoja na mabadiliko katika tasnia ya filamu.Utafiti huu ulibaini kuwa , mvutano una athari chanya na hasi ambapo watafiti walitaja kuwa upotoshwaji wa jamii, kuijenga na kuielimisha jamii, kukuza migogoro, kupoteza imani kuchochea ugaidi pamoja na kudumaza uwezo wa kufikiri. Utafiti huu umesaidia kugundua vyanzo vya maarifa ya kisanaa kwa watunzi ambavyo ni vya kijaala na kijarabati vilevile.Aidha , ujaala ulionekana kutawala zaidi pamoja na kuwa sayansi na teknolojia inaaminika kutawala zaidi kwenye kila Nyanja ya maisha katika karne hii ya sasa. Utafiti umependekeza kuwapo kwa chombo kitakachohakiki kazi za watunzi kifalsafa .Chombo hicho kiwe na wataalamu wa ujenzi wa hoja na uchujaji wa hoja ili kulinda maarifa ya jamii na falsafa yake.Utafiti umebaini pia ufaafu wa nadharia ya semiotiki itumikapo pamoja na nadharia ya mwitiko wa msomaji katika kuchambua filamu nma vipengele vyake.Kutokana na ushikamani na ukamilishani wa nadharia hizi, utafiti huu umependekeza nadharia changamani kwa jina la semioiki-Mwitiko

About Library

The University of Dar es Salaam Library is a vital source of scholarly information that facilitates users to get access to learning and research resources during their studies. It provides access to a wide range of resources in both print and digital formats and conducive reading environment for users, regardless of their physical conditions. All registered users are eligible to access library resources and can borrow print materials from general shelves for a specific period of time.

Useful Links

Koha Staff Login

University Research Repository

WebMail

Aris

Book Study Room

Mara Oral History

Hansard

SOCIAL MEDIA

Instagram

Facebook

Twitter

YouTube

WhatsApp

Ask Librarian

Contact Us

Postal Address
P.O.Box 35092
Dar es Salaam

Call Us: +255 22 2410500/9 Ext. 2165 ; Direct line +255 22 2410241

Fax No:: +255 22 2410241

Email:: directorlibrary@udsm.ac.tz

2025 University of Dar es Salaam - University Of Dar Es Salaam Library
Term of use / Privacy Policy