Uchunguzi wa semantiki na taratibu za utoaji wa majina ya kijita
No Thumbnail Available
Date
2013
Authors
Journal Title
Journal ISSN
Volume Title
Publisher
University of Dar es Salaam
Abstract
Utafiti huu unachunguza Semantiki na Taratibu za utoaji wa majina ya Kijita.
Utafiti ulifanyika katika Mkoa wa Mara, Manispaa ya Musoma Mjini; katika kata
za Buhare, Makoko, Mwigobelo Kigera na Nyamatare. Jumla ya watafitiwa 60
walihusishwa katika utafiti huu. Watafitiwa hao walichaguliwa kwa kutumia
sampuli nasibu tabakishi. Data ya utafiti huu ilikusanywa kwa kutumia mbinu za
hojaji, mahojiano na maktabani. Data ilichambuliwa kwa kutumia mkabala wa
maelezo. Nadharia ya tendo uneni ya Austin (1962) na nadharia jumuishi ya
Uumbaji ya Sapir na Whorf (1958) zilitumika kuongoza utafiti huu. Utafiti huu
umebaini kuwa majina ya Kijita hayatolewi kiholela bali yanafuata taratibu
mbalimbali zilizofumbata falsafa, mila na desturi za Kijita. Utafiti umebaini kuwa
maana za majina mengi ya Kijita zimekitwa katika kazi, matukio, vyakula,
vitoweo na unasibishi wa majina ya wanyama. Vilevile utafiti umebaini kuwa
sababu zinazoukilia majina ya Kijita zimefungamana sana na maana za majina
hayo. Kwa mfano, jina Bulenga (me) lina maana ya mvivu. Sababu iliyochochea
mtu huyu kuitwa jina hili ni tabia ya uvivu aliokuwa nao mtu mwenye jina hili
au mmojawapo wa wazazi wake. Halikadhalika, utafiti umebaini kuwa majina ya
Kijita yanakabiliwa na changamoto mbalimbali katika utoaji na matumizi yake
katika jamii. Aidha, utafiti umebaini kuwa changamoto zinazokabili majina ya
Kijita zinaweza kukabiliwa kwa pamoja kijamii kwa kutoa elimu juu ya umuhimu
wa kutumia majina ya asili, kufahamu maana na sababu za majina hayo pamoja
na taratibu za utoaji na utumiaji wa majina hayo.
Description
Available in print form
Keywords
Jita language, Semantics
Citation
Nyangaywa, M (2013) Uchunguzi wa semantiki na taratibu za utoaji wa majina ya kijita, Tasnifu ya M.A. Kiswahili, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. (Kinapatikana http://41.86.178.3/internetserver3.1.2/search.aspx)