Usawiri wa wahusika wa kike katika hadithi fupi za watoto za kiswahili

dc.contributor.authorMhawili, Angela Peter
dc.date.accessioned2020-04-01T08:00:50Z
dc.date.available2020-04-01T08:00:50Z
dc.date.issued2012
dc.descriptionAvailable in print form, East Africana Collection, Dr. Wilbert Chagula Library, Class mark (THS EAF PL8704.A2M4752)en_US
dc.description.abstractUtaflti huu unashughulikia usawiri wa uhusika wa wanawake katika hadithi fupi za watoto za Kiswahili. Tatizo lililotusukuma kuitafiti mada hiyo linatokana na ukweli kwamba usawiri wa wanawake katika hadithi fupi za watoto haujaguswa bado. Ingawa watoto ni sehemu muhimu ya jamii na ndio wanaohitajika katika kubadili na kuijenga upya jamii, bado suala la malezi yao halijatambulika na kufanyiwa uchunguzi wa kina. Ili kubaini na kuweka wazi suala la malezi ya watoto, tasnifu hii imejikita katika kutafiti juu ya usawiri wa wahusika wa kike katika hadithi fupi za watoto. Hadithi zilizotumika kuchambua tatizo la utaflti zinatoka katika Mradi wa Vitabu vya Watoto Tanzania. Ili kuyatimiza malengo ya utaflti husika, marejeo mbalimbali yalitumika kutoka maktabani. Hivyo utaflti huu ulikuwa wa maktabani. Pia nyenzo za kama vile kompyuta, kalamu na kalatasi, zilitumika katika kukusanyia na kuchambulia data. Mbali na mbinu hizi, mtafiti aliongozwa na nadharia za Mtazamo-Kike kama ilivyorejelewa na Njogu na Chimerah (2008). Katika tasnifu hii imebainika kuwa suala la unyanyasaji na ubaguzi wa kijinsia kwa mtoto wa kike na mwanamke limejitokeza pia katika hadithi fupi za watoto. Tasnifu hii imependekeza kuwa, ili kuibadilisha jamii kutokana na mitazamo potofu dhidi ya jinsia ya kike, na kujenga jamii yenye kufuata misingi ya haki na usawa kwa jinsia zote, watunzi wa kazi za fasihi ya Kiswahili kwa watoto washiriki katika suala la malezi ya watoto kwa kuonyesha usawa wa jinsia kwa wahusika wote.en_US
dc.identifier.citationMhawili, A P (2012) Usawiri wa wahusika wa kike katika hadithi fupi za watoto za kiswahili, Master dissertation, University of Dar es Salaam. Dar es Salaamen_US
dc.identifier.urihttp://41.86.178.5:8080/xmlui/handle/123456789/8660
dc.language.isootheren_US
dc.publisherUniversity of Dar es Salaam,en_US
dc.subjectShort Storiesen_US
dc.subjectSwahilien_US
dc.subjectSwahili languageen_US
dc.subjectWomenen_US
dc.titleUsawiri wa wahusika wa kike katika hadithi fupi za watoto za kiswahilien_US
dc.typeThesisen_US

Files

Original bundle
Now showing 1 - 1 of 1
Loading...
Thumbnail Image
Name:
Angela Peter Mhawili.pdf
Size:
5.98 KB
Format:
Adobe Portable Document Format
Description:
License bundle
Now showing 1 - 1 of 1
No Thumbnail Available
Name:
license.txt
Size:
1.71 KB
Format:
Item-specific license agreed upon to submission
Description: