Repository logo
  • English
  • Català
  • ÄŒeÅ¡tina
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • LatvieÅ¡u
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Log In
    New user? Click here to register. Have you forgotten your password?
Repository logo
    Communities & Collections
    All of DSpace
  • English
  • Català
  • ÄŒeÅ¡tina
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • LatvieÅ¡u
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Log In
    New user? Click here to register. Have you forgotten your password?
  1. Home
  2. Browse by Author

Browsing by Author "Suleiman, Habiba Abdalla"

Now showing 1 - 1 of 1
Results Per Page
Sort Options
  • Loading...
    Thumbnail Image
    Item
    Tofauti za visawe vya nomino za Kiswahili kati ya Tanzania Bara na Zanzibar.
    (University of Dar es Salaam, 2016) Suleiman, Habiba Abdalla
    Utafiti huu unahusu tofauti za visawe vya nomino za Kiswahili kati ya Tanzania Bara na Zanzibar. Data iliyojadiliwa katika utafiti huu imekusanywa kutoka Mikoa mitatu, ambayo ni Dar es Salaam kwa upande wa Tanzania Bara, na kwa upande wa Zanzibar ni Mkoa wa Mjini na Mkoa wa Kusini Pemba. Pia, malengo mahususi matatu yameainishwa ambayo ni: Kuainisha aina za visawe vya nomino za Kiswahili ambao unapatikana kati ya Tanzania Bara na Zanzibar, kujadili sababu zinazochangia tofauti za visawe hivyo pamoja na kufafanua athari zinazoweza kujitokeza kutokana na tofauti hizo. Utafiti huu umehusisha watoa taarifa 25 kutoka kila mkoa na kufanya sampuli kuwa na watoa taarifa 75. Data za utafiti huu zimekusanywa maktabani na uwandani ambapo kwa upande wa data za uwandani mbinu za hojaji na usaili zimetumika. Utafiti huu umeongozwa na Nadharia ya Uhusiano wa Maana iliyoasisiwa na Lyons inayodai kuwa, hakuna vipashio vinavyoweza kuwepo nje ya uhusiano wa vipashio vingine, ambapo nadharia hii imetoa uangavu mkubwa katika kuchanganua vipashio vinavyohusiana na kutofautiana katika utafiti huu. Matokeo ya utafiti yanaonesha kwamba kuna visawe kamili na visawe visivyo kamili, ambapo visawe kamili vinaweza kutoana katika mazingira yote, wakati visawe visivyo kamili haviwezi kutoana sehemu zote katika tungo. Miongoni mwa sababu zilizojadiliwa ambazo husababisha tofauti za msamiati wa visawe ni pamoja na ukopaji wa msamiati, makundi rika katika jamii na jinsia, tofauti za kilahaja na mwingiliano wa lugha moja na nyingine. Vilevile, utafiti umebaini kuwepo kwa tofauti hizo kuna athari ambazo zinajitokeza zikiwemo kutoelewana, utambulisho, kukua kwa lugha na mfumuko wa visawe. Aidha, katika utafiti huu, yametolewa mapendekezo kadhaa. Kwanza, utafiti unaweza kufanywa kwa kuchunguza kategoria nyingine za maneno kama vile: vitenzi, vielezi, viunganishi, vihusishi na vihisishi ili kubaini iwapo kuna tofauti za kimatamshi, maumbo na matumizi ya maneno katika lugha ya Kiswahili kwa Tanzania Bara na Zanzibar. Pili, utafiti kama huu unaweza kufanywa katika maeneo mengine yanayotumia lugha hii kama vile Kenya, Uganda, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Visiwa vya Komoro. Tatu, uchunguzi unaweza kufanywa ili kubaini maneno ambayo yana maumbo sawa lakini yana maana tofauti kati ya Tanzania Bara na Zanzibar.

About Library

The University of Dar es Salaam Library is a vital source of scholarly information that facilitates users to get access to learning and research resources during their studies. It provides access to a wide range of resources in both print and digital formats and conducive reading environment for users, regardless of their physical conditions. All registered users are eligible to access library resources and can borrow print materials from general shelves for a specific period of time.

Useful Links

Koha Staff Login

University Research Repository

WebMail

Aris

Book Study Room

Mara Oral History

Hansard

SOCIAL MEDIA

Instagram

Facebook

Twitter

YouTube

WhatsApp

Ask Librarian

Contact Us

Postal Address
P.O.Box 35092
Dar es Salaam

Call Us: +255 22 2410500/9 Ext. 2165 ; Direct line +255 22 2410241

Fax No:: +255 22 2410241

Email:: directorlibrary@udsm.ac.tz

2025 University of Dar es Salaam - University Of Dar Es Salaam Library
Term of use / Privacy Policy