Repository logo
  • English
  • Català
  • Čeština
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • Latviešu
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Log In
    New user? Click here to register. Have you forgotten your password?
Repository logo
    Communities & Collections
    All of DSpace
  • English
  • Català
  • Čeština
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • Latviešu
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Log In
    New user? Click here to register. Have you forgotten your password?
  1. Home
  2. Browse by Author

Browsing by Author "Stephen, Selina"

Now showing 1 - 1 of 1
Results Per Page
Sort Options
  • Loading...
    Thumbnail Image
    Item
    Uchambuzi wa maana na dhima za sitiari katika maandishi ya bajaji
    (University of Dar es Salaam, 2019) Stephen, Selina
    Utafiti huu ulilenga kuchunguza maana na dhima za sitiari zitokeazo kwenye maandishi ya bajajini. Utafiti huu umefanyika katika Mkoa wa Dar es Salaam, Wilaya za Kinondoni na Ubungo. Katika wilaya ya Kinondoni utafiti ulifanyika katika kata za Kinondoni na Kawe: na katika Wilaya ya Ubungo, utafiti ulifanyika katika kata ya Ubungo. Mbinu za utafiti zilihusisha uteuzi wa sampuli na usampulishaji, mbinu za ukusanyaji data na mbinu za uchambuzi wa data. Data ya utafiti iliyohusika katika utafiti huu ni maandishi yaliyoandikwa kwenye bajaji yaliyokusanywa na mtafiti kutoka uwandani. Watafitiwa walisailiwa ili kupata dhima ya sitiari zilizobainishwa. Utafiti huu pia ulitumia data za maktabani, zinazohusu sitiari. Kazi hii imegawanyika katika sura tano. Sura ya kwanza imetoa maelezo ya kiini cha tatizo na mbinu ambazo zimetumika katika kufikia mahitimisho. Sura ya tatu imezungumzia na kujadili mbinu mbalimbali za utafiti ambazo ni sampuli na usambulishaji, mbinu za kukusanya data na mbinu zilizotumika kuchanganua data. Sura ya nne imeshughulikia uwasilishaji na uchanganuzi wa data. Data za uwandani zimechanganuliwa kwa njia ya maelezo na majedwali. Uchanganuzi huu wa data umeongozwa na “Nadharia ya Maana kama Matumizi. “Nadharia hii imeasisiwa na mwanafalsafa Wittgenstein (1953). Msingi wake mkuu umejikita katika kusistiza kuwa “maana ya neno iko katika matumizi yake.” Na lugha hufungamanishwa na tabia za binadamu na namna wanavyohusiana baina yao. Kwa jumla, matumizi”. Sura ya tano imeshughulikia matokeo ya utafiti, hitimisho na mapendekezo ya utafiti fuatishi. Matokeo ya utafiti yambainisha kuwa maana za sitiari hupatikana kwa kuzingatia muktadha unaohusika. Huwezi kupata maana bila kujua sababu, lengo na makusudio ya sitiari hiyo. Maana inayohamishwa hutegemea muktadha unaohusisha tukio. Vilevile, lengo kubwa la dhima zilizopatikana katika sitiari hizo ni kuwaasa na kuwakumbusha wanadamu jinsi ya kuishi katika jamii. Kutokana na matokeo hayo tunajifunza kuwa huwezi kupata maana nje ya muktadha unaohusika. Utafiti pia unapendekeza kuwa huwezi kupata maana nje ya muktadha unaohusika. Utafiti pia unapendekeza kuwa tafiti fuatizi zifanyike kuhusu (a) kutotumika sana kwa sitiari katika maandishi ya bajaji, na (b) uhusiano baina ya maana na dhima za sitiari.

About Library

The University of Dar es Salaam Library is a vital source of scholarly information that facilitates users to get access to learning and research resources during their studies. It provides access to a wide range of resources in both print and digital formats and conducive reading environment for users, regardless of their physical conditions. All registered users are eligible to access library resources and can borrow print materials from general shelves for a specific period of time.

Useful Links

Koha Staff Login

University Research Repository

WebMail

Aris

Book Study Room

Mara Oral History

Hansard

SOCIAL MEDIA

Instagram

Facebook

Twitter

YouTube

WhatsApp

Ask Librarian

Contact Us

Postal Address
P.O.Box 35092
Dar es Salaam

Call Us: +255 22 2410500/9 Ext. 2165 ; Direct line +255 22 2410241

Fax No:: +255 22 2410241

Email:: directorlibrary@udsm.ac.tz

2025 University of Dar es Salaam - University Of Dar Es Salaam Library
Term of use / Privacy Policy