Repository logo
  • English
  • Català
  • ÄŒeÅ¡tina
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • LatvieÅ¡u
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Log In
    New user? Click here to register. Have you forgotten your password?
Repository logo
    Communities & Collections
    All of DSpace
  • English
  • Català
  • ÄŒeÅ¡tina
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • LatvieÅ¡u
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Log In
    New user? Click here to register. Have you forgotten your password?
  1. Home
  2. Browse by Author

Browsing by Author "Ramadhan, Sakina Khamis"

Now showing 1 - 1 of 1
Results Per Page
Sort Options
  • No Thumbnail Available
    Item
    Usawiri wa mwanamke katika taarab ya mipasho: mfano kutoka nyimbo za mzee Yussuf Mzee
    (Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, 2013) Ramadhan, Sakina Khamis
    Lengo kuu la utafiti huu lilikuwa ni kuchunguza usawiri wa mwanamke katika nyimbo za taarab ya mipasho za Mzee Yussuf Mzee. Malengo mahsusi yalikuwa ni manne nayo ni kubainisha usawiri wa mwanamke katika nyimbo za taarab ya mipasho za Mzee Yussuf, kueleza aina ya usawiri wa mwanamke inayojitokeza zaidi katika nyimbo hizo za taarab ya mipasho za msanii teule, kubainisha sababu zinazofanya mwanamke asawiriwe hivyo na kueleza uhusiano baina ya hadhi aliyopewa mwanamke katika nyimbo za taarab ya mipasho za msanii huyu na hali halisi ya mwanamke wa Tanzania. Nadharia ya Ufeministi ilitumika katika uchambuzi wa data wa tasnifu hii. Mbinu za ukusanyaji wa data maktabani kwa kusoma maandiko na machapisho mbalimbali na uwandani zilitumika katika utafiti huu. Kwa upande wa mbinu za uwandani, tulitumia mbinu ya ushuhudiaji, usaili, hojaji na usikilizaji wa vipindi vya taarab redioni na katika televisheni. Matokeo ya utafiti yanaonesha kwamba Mzee Yussuf Mzee anamsawiri mwanamke katika namna mbalimbali kama vile chombo cha starehe cha mwanaume, kiumbe mwenye heshima, mnyenyekevu na mpole, mvumilivu na mwaminifu, mficha siri, mshauri na mlezi wa familia. Kwa ujumla, utafiti wetu umebaini kwamba usawiri wa mwanamke kama chombo cha starehe kwa mwanaume na mwanamke kama pambo ndio unaojitokeza zaidi kuliko aina nyingine ya usawiri. Utafiti wetu umebaini kwamba miongoni mwa mambo yanayofanya msanii amsawiri mwanamke hivyo ni mahitaji ya soko la muziki wa taarab, mapenzi ya Mzee Yussuf kwa wanawake, mwanamke mwenyewe, utamaduni, mila na desturi na utekelezaji dhaifu wa sera za masuala ya jinsia nchini. Pia, utafiti umebaini kwamba hadhi anayopewa mwanamke katika nyimbo za Mzee Yussuf haifanani na mwanamke halisi wa Kitanzania katika jamii.

About Library

The University of Dar es Salaam Library is a vital source of scholarly information that facilitates users to get access to learning and research resources during their studies. It provides access to a wide range of resources in both print and digital formats and conducive reading environment for users, regardless of their physical conditions. All registered users are eligible to access library resources and can borrow print materials from general shelves for a specific period of time.

Useful Links

Koha Staff Login

University Research Repository

WebMail

Aris

Book Study Room

Mara Oral History

Hansard

SOCIAL MEDIA

Instagram

Facebook

Twitter

YouTube

WhatsApp

Ask Librarian

Contact Us

Postal Address
P.O.Box 35092
Dar es Salaam

Call Us: +255 22 2410500/9 Ext. 2165 ; Direct line +255 22 2410241

Fax No:: +255 22 2410241

Email:: directorlibrary@udsm.ac.tz

2025 University of Dar es Salaam - University Of Dar Es Salaam Library
Term of use / Privacy Policy