Repository logo
  • English
  • Català
  • ÄŒeÅ¡tina
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • LatvieÅ¡u
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Log In
    New user? Click here to register. Have you forgotten your password?
Repository logo
    Communities & Collections
    All of DSpace
  • English
  • Català
  • ÄŒeÅ¡tina
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • LatvieÅ¡u
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Log In
    New user? Click here to register. Have you forgotten your password?
  1. Home
  2. Browse by Author

Browsing by Author "Pacho, Peter Jacobo"

Now showing 1 - 1 of 1
Results Per Page
Sort Options
  • Loading...
    Thumbnail Image
    Item
    Athari ya mhariri katika mswada: uchunguzi wa machapisho teule ya kifasihi ya Kiswahili
    (University of Dar es Salaam, 2017) Pacho, Peter Jacobo
    Utafiti huu umelenga kuchunguza Athari ya Mhariri katika Miswada ya Kifasihi ya Kiswahili. Hii inatokana na kuwapo kwa malalamiko mengi kutoka kwa baadhi ya waandishi juu ya namna wahariri wanavyohariri miswada yao. Malalamiko hayo husababisha kuwapo kwa mgongano baina ya wahariri na waandishi. Hoja ya msingi katika utafiti huu ni kuwa mhariri ni kiungo muhimu sana katika tasnia ya uchapishaji licha ya kuwapo kwa dosari ndogondogo zinazojitokeza kwa wahariri wasiokuwa makini. Mtafiti ameongozwa na malengo mahususi, yaani kubaini sifa za mhariri wa miswada ya kifasihi ya Kiswahili, kufafanua majukumu ya mhariri wa miswada ya kifasihi ya Kiswahili na jinsi anavyozingatia majukumu yake na kubainisha athari za mhariri katika miswada ya kifasihi ya Kiswahili. Katika ukusanyaji wa data za uwandani na maktabani katika wilaya za Kinondoni, Ubungo na Ilala, mtafiti ametumia mbinu za mahojiano na uchambuzi na uchanganuzi wa matini teule. Kwa kutumia Nadharia ya Mwitiko wa Msomaji, Nadharia ya Uhariri na baadhi ya Kanuni za Uhariri zimeweza kubainika athari chanya na athari hasi za mhariri. Athari chanya ni kuboresha lugha ya mwandishi; kuboresha msuko wa hadithi na kuboresha maudhui ya kitabu. Kwa upande mwingine athari hasi ni kubadili jina na umbo la kitabu; kucheleweshwa kwa miswada; athari za kidhana na kimaana; kubadili sauti ya mwandishi na kukosekana kwa ushikamani, uthabiti na muwala. Licha ya kuwapo kwa malalamiko mengi ya waandishi juu ya namna wahariri wanavyohariri kazi zao, na kuonesha kuwa kwa sehemu kubwa wahariri wanaharibu miswada yao. Mtafiti amegundua kuwa mengi ya malalamiko hayo siyo ya msingi, na yanatokana na waandishi wengi kutokuwa na uelewa wa kutosha kuhusiana na taaluma ya uchapishaji, hususan kipengele cha uhariri.

About Library

The University of Dar es Salaam Library is a vital source of scholarly information that facilitates users to get access to learning and research resources during their studies. It provides access to a wide range of resources in both print and digital formats and conducive reading environment for users, regardless of their physical conditions. All registered users are eligible to access library resources and can borrow print materials from general shelves for a specific period of time.

Useful Links

Koha Staff Login

University Research Repository

WebMail

Aris

Book Study Room

Mara Oral History

Hansard

SOCIAL MEDIA

Instagram

Facebook

Twitter

YouTube

WhatsApp

Ask Librarian

Contact Us

Postal Address
P.O.Box 35092
Dar es Salaam

Call Us: +255 22 2410500/9 Ext. 2165 ; Direct line +255 22 2410241

Fax No:: +255 22 2410241

Email:: directorlibrary@udsm.ac.tz

2025 University of Dar es Salaam - University Of Dar Es Salaam Library
Term of use / Privacy Policy