Repository logo
  • English
  • Català
  • ÄŒeÅ¡tina
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • LatvieÅ¡u
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Log In
    New user? Click here to register. Have you forgotten your password?
Repository logo
    Communities & Collections
    All of DSpace
  • English
  • Català
  • ÄŒeÅ¡tina
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • LatvieÅ¡u
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Log In
    New user? Click here to register. Have you forgotten your password?
  1. Home
  2. Browse by Author

Browsing by Author "Ninsiima, Betty"

Now showing 1 - 1 of 1
Results Per Page
Sort Options
  • Loading...
    Thumbnail Image
    Item
    Changamoto zinazowakabili wanafunzi wa sekondari wanapotafsiri kutoka kiingereza hadi Kiswahili
    (Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, 2017) Ninsiima, Betty
    Utafiti huu kuhusu Changamoto zinazowakabili wanafunzi wa sekondari nchini Uganda wanapotafsirimatinikutokaKiingerezahadiKiswahiliunakusudiwakupunguzachangamotozakutafsirimatinikutokaKiingerezahadiKiswahili. Utafitiulikuwanamalengomawiliyafuatayo: Kwanza, kubainisha changamoto zinazowakabili wanafunzi wanapotafsiri matini kutoka Kiingereza hadi Kiswahili. Lengo la pili lilikuwa kuchunguza chanzo cha changamoto zinazowakabili wanafunzi wanapotafsiri matini kutoka Kiingereza hadi Kiswahili. Kutokana na uchunguzi watoa tarifa walitoa mapendekezo na mikakati ya kupunguza changamoto zinazowakabili wanafunzi wanapotafsiri matini kutoka Kiingereza hadi Kiswahili, ambalo ni lengo la tatu. Katika utafiti huu, mtafiti alitumia hojaji na mahojiano kukusanya data aliyotumia kujibu maswali yake ya utafiti. Ufafanuziwa data na matokeo ulifanywa kwa kutumia mkabala wa kimaelezo na kiidadi. Nadharia ya Ulinganifu Matini ndio iliyotumika katika utafitihuu. Matokeo ya utafiti huu yanadhihirisha kwamba kuna changamoto nyingi katika kutafsiri matini kutoka Kiingereza hadi Kiswahili kwa wanafunzi wasekondari. Uchunguzi unaonyesha kwamba kuna changamoto ya kukosa msamiati wa kutumia wakati wanapotafsiri matini kutoka Kiingereza hadi Kiswahili, ukosefu wa vitabu vya kutosha vya kutumia, athari za lugha mama na kadhalika. Mikakati mingi ilipendekezwa kupunguza changamoto hizi. Mapendekezo ya Wanafunzi: vitabu vinavyofaavya Kiswahili viwekwe kwenye maktaba, walimu wa Kiswahili wasahihishe kazi zao kila wakati ili waweze kuwarekebisha wanaposhindwa, Kiswahili kama Kiingereza kifundishwe kuanzia shule za msingi, nawanafunzi wanaofaulu kutunukiwa. Walimu pia walipendekeza yafuatayo: kuwepo sera nzuri zinazoeleweka na kuianzisha lugha hii ya Kiswahili katika shule na vipimo viwekwe ili wanafunzi wapunguze utumiaji wa lugha za mitaani na zakienyeji, wapate kozi za kukuza lugha, vipindi vya Kiswahili darasani viongezwe, serikali iwaajiri walimu wa Kiswahili wakutosha na kutoaf edha za kununua vitabu vinavyofaa na vifaa vingine vya kujifunza na kufundishia lugha ya Kiswahili, kunahitajika programu za ufundishaji wa walimu wa Kiswahili ambazo zitawachangamsha na kuleta nguvu mpya na kutengeneza upya mielekeo mipya katika ujifunzaji na utafsiri wa matini za Kiingereza kwenda Kiswahili kwa jumla. Pia, walimuwa Kiswahili wanapaswa kupanua mbinu za kufundisha na kuchangamsha masomo yao ili yapendeze kwa wanafunzi wao. Majukumu ya Serikali: inastahili kuifanya Kiswahili lugha rasmi ya pili ya nchi ili kila Mganda aongee lugha hii jambo ambalo litawasaidia wanafunzi kupanua msamiati katika lugha. Wizara ya Elimu ikuze na kuweka katika mtalaa wa nchi silabasi ya kuanzisha na kufundisha Kiswahili kuanzia shule za msingi.

About Library

The University of Dar es Salaam Library is a vital source of scholarly information that facilitates users to get access to learning and research resources during their studies. It provides access to a wide range of resources in both print and digital formats and conducive reading environment for users, regardless of their physical conditions. All registered users are eligible to access library resources and can borrow print materials from general shelves for a specific period of time.

Useful Links

Koha Staff Login

University Research Repository

WebMail

Aris

Book Study Room

Mara Oral History

Hansard

SOCIAL MEDIA

Instagram

Facebook

Twitter

YouTube

WhatsApp

Ask Librarian

Contact Us

Postal Address
P.O.Box 35092
Dar es Salaam

Call Us: +255 22 2410500/9 Ext. 2165 ; Direct line +255 22 2410241

Fax No:: +255 22 2410241

Email:: directorlibrary@udsm.ac.tz

2025 University of Dar es Salaam - University Of Dar Es Salaam Library
Term of use / Privacy Policy