Repository logo
  • English
  • Català
  • Čeština
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • Latviešu
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Log In
    New user? Click here to register. Have you forgotten your password?
Repository logo
    Communities & Collections
    All of DSpace
  • English
  • Català
  • Čeština
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • Latviešu
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Log In
    New user? Click here to register. Have you forgotten your password?
  1. Home
  2. Browse by Author

Browsing by Author "Moshi, Lioba"

Now showing 1 - 1 of 1
Results Per Page
Sort Options
  • Loading...
    Thumbnail Image
    Item
    Ulinganisho wa vikundi nomino vya Kiswahili na Kivunjo
    (Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, 1976) Moshi, Lioba
    Madhumuni ya tasnifu hii ni kujaribu kulinganisha lugha mbili za Kibantu:- Kivunjo lugha ya kuzaliwa na Kiswahili lugha ya pili. Katika lugha hizi mbili, uchunguzi wake bado ni duni sana, kwa hiyo mengi yatakayojitokeza ni kutokana na juhudi za kibinafsi katika kutafuta na kupekuwa maandishi mbalimbali kuhusu lugha kwa ujumla nay ale machache yaliyowahi kuandikwa kuhusu Kiswahili na lugha nyingine za Kibantu. Mengine pia yametokana na watumiaji wa lugha hizi, mimi binafsi nikiwa mmojawapo. Watumiji wa lugha ya Kiswahili ni wakazi wa Tanzania na baadhi ya nchi za jirani. Niliohusu nao hapa ni watanzania tu. Watumiaji wa Kivunjo ni kikundi cha wachagga waishio kwenye miteremko yam lima Kilimanjaro katika wilaya ya Moshi, katikati ya wilaya za Hai na Rombo. Wenyewe hawakiiti Kivunjo, bali “Kianjo” kutokana na wakazi wake, Waanjo. Hawa ni watu waishio sehemu za Kirua, Kilema, Marangu, Mamba na Mwika. Wamochi wakaao sehemu ijulikanayo kama “Old Moshi” nao pia hutumia kilugha hiki ingawaje tofauti zilizopo kati ya watumiaji wa sehemu hizi nyingine. Tofauti hizo sitaziingilia katika tasnifu hii ila nitajishughulisha na Kivunjo kama watumiavyo Waanjo wa Kirua Vunjo – sehemu Kivunjo na Kiswahili. Hii itafanyika kama ifuatavyo. 1. Uchunguzi kuhusu ngeli za majina. Hapa dhana mbalimbali za wanaisimu zimejitokeza . Nadharia iliyotumika hasa ni ile ya upatanisho wa Kisarufi na utumiaji hasa ni ile ya upatanisho wa Kisarufi na utumiaji wa namba, kuainisha ngeli hizo. Vipengele vinginevyo vihusuvyo dhana ya ngeli pia vimejadiliwa. Matatizo yatajitokeza katika uchambuzi huu hasa katika Kivunjo ingawaje hayataelezwa kwa kirefu sana. 2. Uchambuzi wa vikundi nomino vyenyewe katika usawia wa vipashio muhimu K (Kisifio) Sh (Shina) na S (sifa).Sehemu hii ndio itakayokuwa muhimu kwa sababu inahusika zaidi katika tasnifu hii katika kivajadili vikundi nomino vya lugha hizi mbili: Nadharia ya “Scale and Categories of Grammar” ya Halliday (1961) ndio itakayotumika katika kujaribu kutekeleza lengo hili. Matatizo yatokanayo nayo yataelezwa pahitajipo. 3. Mahitimisho –sehemu hii itaonyesha marejeo ya kazi yote na kujaribu kuzilinganisha lugha hizi mbili: Muundo na mpangilio wa vikundi nomino ndiyo mambo yatakayo shughulikiwa katika ulinganisho huu, ulingano na tofati zikionyeshwa kwa maelezo mafupi iwezekanavyo. Kufaulu na kutofaulu ni sehemu ndogo pia itakayojitokeza hapa katika kuchambua vikundi nomino na vipashio vyake kwa kutumia nadharia itakayopendekezwa. Sababu zilizokuwa dhahiri zitatajwa, pasipowezekana, mapendekezo yatatolewa.

About Library

The University of Dar es Salaam Library is a vital source of scholarly information that facilitates users to get access to learning and research resources during their studies. It provides access to a wide range of resources in both print and digital formats and conducive reading environment for users, regardless of their physical conditions. All registered users are eligible to access library resources and can borrow print materials from general shelves for a specific period of time.

Useful Links

Koha Staff Login

University Research Repository

WebMail

Aris

Book Study Room

Mara Oral History

Hansard

SOCIAL MEDIA

Instagram

Facebook

Twitter

YouTube

WhatsApp

Ask Librarian

Contact Us

Postal Address
P.O.Box 35092
Dar es Salaam

Call Us: +255 22 2410500/9 Ext. 2165 ; Direct line +255 22 2410241

Fax No:: +255 22 2410241

Email:: directorlibrary@udsm.ac.tz

2025 University of Dar es Salaam - University Of Dar Es Salaam Library
Term of use / Privacy Policy