Repository logo
  • English
  • Català
  • ÄŒeÅ¡tina
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • LatvieÅ¡u
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Log In
    New user? Click here to register. Have you forgotten your password?
Repository logo
    Communities & Collections
    All of DSpace
  • English
  • Català
  • ÄŒeÅ¡tina
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • LatvieÅ¡u
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Log In
    New user? Click here to register. Have you forgotten your password?
  1. Home
  2. Browse by Author

Browsing by Author "Masuba, Shida"

Now showing 1 - 1 of 1
Results Per Page
Sort Options
  • No Thumbnail Available
    Item
    Je, Kinyakyusa kina mkazo au toni?
    (University of Dar es Salaam, 2013) Masuba, Shida
    Wataalamu wengi wa fonolojia, wanaelekea kukubaliana kwamba Lugha za ki-Bantu ziko katika makundi manne: lugha zenye toni asilia, lugha zenye viinitoni, lugha zilizo kati ya kuwa na viinitoni na kuwa na mkazo na lugha zenye mkazo peke yake. (taz. McCawley 1974 na Massamba 2011:176-177). Hata hivyo, ni lugha chache zilizochunguzwa vipambasauti vyake vya toni na mkazo, na kubainika kuwa kuna lugha zenye toni asilia, viinitoni na mkazo peke yake, lakini lugha zenye viinitoni na mkazo hakuna iliyobainika katika kundi hilo. Hivyo, utafiti huu unahusu mkazo na toni katika kiwango cha neno na tungo katika Kinyakyusa ili kuziba pengo hili. Data zilizotumika ni nomino, vivumishi, vitenzi, viwakilishi na vielezi, pamoja na tungo virai na sentensi zilizokusanywa katika kijiji cha Ibula, Kasyeto na Lwifwa tarafa ya Ukukwe, Msasani na Pakati Wilayani Rugwe, Mkoani Mbeya. Data zilikusanywa kwa njia za mahojiano, ushiriki na ushuhudiaji kisha kurekodiwa kwa kinasasauti. Katika uchanganuzi wa data tumetumia nadharia ya FM iliyoasisiwa na Liberman & Prince (1977) na FVH iliyoasisiwa na Goldsmith (1976) ambapo vipengele vya kifonolojia vimewakilishwa katika rusu huru. Utafiti huu umegusia vipengelele vya vya irabu, konsonanti, silabi na mambo yanayodhibiti ruwaza za mkazo na toni. Aidha, imebainika kuwa Kinyakyusa kina mkazo huru, unaoangukia silabi yoyote katika neno na katika kiwango cha tungo, kikonyo dada cha pili kina nguvu kuliko cha kwanza katika kategoria ya kirai na kileksika. Vilevile, imebainika kuwa Kinyakyusa kina maegemeomkazo huru na funge. Kwa upande mwingine imebainika kuwa Kinyakyusa kina toni zinazochombezwa na kiinitoni. Kiinitoni chake kinahusishwa na tonijuu. KTM cha nomino za lugha hii ni JC, CJC na CJ, na CJC kwa upande wa vitenzi. Aidha, kuna kanuni zimejibainisha, nazo ni: upachikaji kiinitoni, udondoshaji wa kiinitoni, mbiruko nyuma wa kiinitoni na usambaaji tonijuu kulia na kanuni za uhusishaji KTM na kiinitoni. Matokeo ya utafiti huu yanakanusha madai yanayosema: lugha ya Kinyakyusa ina mkazo peke yake na haina toni, bali unaonesha kuwa lugha ya Kinyakyusa ina mkazo na toni na hivyo kuingia katika kundi la tatu la lugha za Kibantu lenye lugha ambazo ziko kati ya kuwa na viinitoni na kuwa na mkazo.

About Library

The University of Dar es Salaam Library is a vital source of scholarly information that facilitates users to get access to learning and research resources during their studies. It provides access to a wide range of resources in both print and digital formats and conducive reading environment for users, regardless of their physical conditions. All registered users are eligible to access library resources and can borrow print materials from general shelves for a specific period of time.

Useful Links

Koha Staff Login

University Research Repository

WebMail

Aris

Book Study Room

Mara Oral History

Hansard

SOCIAL MEDIA

Instagram

Facebook

Twitter

YouTube

WhatsApp

Ask Librarian

Contact Us

Postal Address
P.O.Box 35092
Dar es Salaam

Call Us: +255 22 2410500/9 Ext. 2165 ; Direct line +255 22 2410241

Fax No:: +255 22 2410241

Email:: directorlibrary@udsm.ac.tz

2025 University of Dar es Salaam - University Of Dar Es Salaam Library
Term of use / Privacy Policy