Repository logo
  • English
  • Català
  • ÄŒeÅ¡tina
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • LatvieÅ¡u
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Log In
    New user? Click here to register. Have you forgotten your password?
Repository logo
    Communities & Collections
    All of DSpace
  • English
  • Català
  • ÄŒeÅ¡tina
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • LatvieÅ¡u
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Log In
    New user? Click here to register. Have you forgotten your password?
  1. Home
  2. Browse by Author

Browsing by Author "Mashaka, Asia"

Now showing 1 - 1 of 1
Results Per Page
Sort Options
  • No Thumbnail Available
    Item
    Ruwaza na maana za utendeka na utendana katika vitenzi vya Kihehe
    (Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, 2013) Mashaka, Asia
    Utafiti huu ulioshughulikia Ruwaza na Maana za Utendeka na Utendana katika lugha ya Kihehe ulifanyika mkoani Iringa katika wilaya ya Mufindi vijiji vya Rungemba, Maduma na Waasa. Malengo ya utafiti yalikuwa ni kubainisha maumbo, mfuatano na maana zinazoukiliwa na mofimu nyambulishi hizo. Data za utafiti huu zilipatikana uwandani kwa watafitiwa wapatao sabini na wawili (72) kwa kutumia mbinu ya ushuhudiaji, mahojiano na hojaji. Aidha, utafiti huu uliongozwa na Kanuni Akisi (KA) ya Baker (1985): Unyambulishaji wa kimofolojia sharti uakisi unyambulishaji wa kisintaksia.Matokeo ya utafiti huu yamebaini kuwa unyambulishaji tendeka katika lugha ya Kihehe unawakilishwa na mofimu //-isik-// katika vitenzi vya silabi moja na mofimu //-ik-// kwa vitenzi viso-ukomo. Aidha, matokeo ya utafiti huu yanabainisha mofimu //-kwi-// na //-an-// kuwa ni maumbo yanayodokeza unyambulishaji tendana katika lugha ya Kihehe. Mofimu //-kwi-// inatokea kabla ya mzizi ilhali mofimu //-an-// hunyambulishwa baada ya mzizi au shina la kitenzi. Vilevile, utafiti huu umeeleza na kuunda kanuni zinazoongoza utokeaji wa unyambulishaji tendeka na tendana. Pia, katika utafiti huu imebainika kuwa mfuatano wa mofimu nyambulishi za utendeka na za utendana haukubaliki. Mfuatano unaokubalika ni ule unaohusu mofimu nyambulishi ya utendana na tendeka //-an- + -ik-// katika vitenzi viso-ukomo, hususani kwa umbo //-an-// pekee. Aidha, matokeo yanaonesha maana zinazodokezwa na mofimu tendeka ni pamoja na uwezekano wa jambo kufanyika na urahisi wa kutenda jambo fulani. Mofimu ya utendana //-kwi-// na //-an-// inahukilia maana ya ushirikiano. Pia, mofimu hizo hufungamana na maana ya kinahau ambapo ili kupata maana huhitaji urejelezi wa muktadha wa kimatumizi. Utafiti pia umependekeza tafiti nyingine kufanyika kuhusu unyambulishaji wa mofimu nyambulishi nyingine ili kubaini maumbo, mfuatano na maana zinazodokezwa na mofimu nyambulishi hizo katika lugha hii.

About Library

The University of Dar es Salaam Library is a vital source of scholarly information that facilitates users to get access to learning and research resources during their studies. It provides access to a wide range of resources in both print and digital formats and conducive reading environment for users, regardless of their physical conditions. All registered users are eligible to access library resources and can borrow print materials from general shelves for a specific period of time.

Useful Links

Koha Staff Login

University Research Repository

WebMail

Aris

Book Study Room

Mara Oral History

Hansard

SOCIAL MEDIA

Instagram

Facebook

Twitter

YouTube

WhatsApp

Ask Librarian

Contact Us

Postal Address
P.O.Box 35092
Dar es Salaam

Call Us: +255 22 2410500/9 Ext. 2165 ; Direct line +255 22 2410241

Fax No:: +255 22 2410241

Email:: directorlibrary@udsm.ac.tz

2025 University of Dar es Salaam - University Of Dar Es Salaam Library
Term of use / Privacy Policy