Repository logo
  • English
  • Català
  • ÄŒeÅ¡tina
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • LatvieÅ¡u
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Log In
    New user? Click here to register. Have you forgotten your password?
Repository logo
    Communities & Collections
    All of DSpace
  • English
  • Català
  • ÄŒeÅ¡tina
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • LatvieÅ¡u
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Log In
    New user? Click here to register. Have you forgotten your password?
  1. Home
  2. Browse by Author

Browsing by Author "Libui, Omari Selemani"

Now showing 1 - 1 of 1
Results Per Page
Sort Options
  • No Thumbnail Available
    Item
    Riwaya mpya ya kiswahili na masuluhisho ya changamoto za utandawazi
    (Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, 2012) Libui, Omari Selemani
    Utafiti huu umechunguza riwaya mpya ya Kiswahili na masuluhisho ya changamoto za utandawazi riwaya teule zikiwa Babu Alipofufuka (2001) na Bina-Adamu! (2002). Utafiti huu umechunguza changamoto mbalimbali za utandawazi, masuluhisho yanayotolewa na waandishi kuhusiana na changamoto za utandawazi na mitazamo ya waandishi katika kukabiliana na changamoto hizo. Ili kufikia lengo hilo, mbinu kuu ya ukusanyaji wa data iliyotumika ni usomaji wa matini. Pamoja na mbinu hiyo, vifaa mbalimbali kama vile kalamu na shajara, kinyonyi na kompyuta vilitumika. Aidha, uchambuzi na ufasili wa data ulielemea katika nadharia ya uhalisia. Matokeo ya utafiti huu yanaonesha kuwa waandishi Mohamed (2001) na Wamitila (2002) wamejadili na kutoa masuluhisho mbalimbali kuhusiana na changamoto za utandawazi. Masuluhisho hayo yapo katika madaraja ya kiuchumi, kisiasa, kiutamaduni, kiteknolojia, kimazingira na ya kijamii kwa ujumla. Lakini tunaweza kusema kwa ujumla wake kuwa masuluhisho haya yamekitwa katika mitazamo ya ndani ya Afrika. Waandishi wanapendekeza kuwa ili Afrika ijinasue kutokana na matatizo mbalimbali yaliyosababishwa na utandawazi basi haina budi kujipanga upya na kuelekeza juhudi zake za pamoja katika kuhakikisha Afrika inajitegemea kwa kila jambo. Aidha suala la msingi linalosisitizwa na waandishi ni kuona Afrika ikichanua yenyewe bila masharti na maelekezo kutoka nchi za Magharibi kupitia vyombo vyao vinavyomiliki mwenendo wa siasa, fedha na uchumi wa kiulimwengu. Mwisho utafiti huu unapendekeza kufanyika tafiti zaidi kuhusiana na mchango wa fasihi andishi ya Kiswahili katika kukabailiana na matatizo ya utandawazi. Aidha, suala la mafungamano baina ya Afrika na nchi zilizoendelea kiuchumi lifanyiwe mjadala wa kutosha. Mwisho viongozi wa kisiasa wa Afrika waamke kutoka usingizini na kusimama imara kutoka na tishio la utandawazi.

About Library

The University of Dar es Salaam Library is a vital source of scholarly information that facilitates users to get access to learning and research resources during their studies. It provides access to a wide range of resources in both print and digital formats and conducive reading environment for users, regardless of their physical conditions. All registered users are eligible to access library resources and can borrow print materials from general shelves for a specific period of time.

Useful Links

Koha Staff Login

University Research Repository

WebMail

Aris

Book Study Room

Mara Oral History

Hansard

SOCIAL MEDIA

Instagram

Facebook

Twitter

YouTube

WhatsApp

Ask Librarian

Contact Us

Postal Address
P.O.Box 35092
Dar es Salaam

Call Us: +255 22 2410500/9 Ext. 2165 ; Direct line +255 22 2410241

Fax No:: +255 22 2410241

Email:: directorlibrary@udsm.ac.tz

2025 University of Dar es Salaam - University Of Dar Es Salaam Library
Term of use / Privacy Policy