Repository logo
  • English
  • Català
  • ÄŒeÅ¡tina
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • LatvieÅ¡u
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Log In
    New user? Click here to register. Have you forgotten your password?
Repository logo
    Communities & Collections
    All of DSpace
  • English
  • Català
  • ÄŒeÅ¡tina
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • LatvieÅ¡u
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Log In
    New user? Click here to register. Have you forgotten your password?
  1. Home
  2. Browse by Author

Browsing by Author "Koroti, Ester"

Now showing 1 - 1 of 1
Results Per Page
Sort Options
  • Loading...
    Thumbnail Image
    Item
    Ufaafu wa mifano ya matumizi kwenye kamusi ya kiswahili sanifu (TUKI, 2013) katika kupata maana ya kidahizo mifano kutoka shule za sekondari
    (University of Dar es Salaam, 2017) Koroti, Ester
    Kamusi inasaidia kuifahamu lugha vizuri kwa kuvitumia vipengele mbalimbali vya kiisimu. Vipengele vinavyoangaliwa kwenye kamusi ni pamoja na maana ya neno, kategoria, matamshi, ngeli za nomino na mifano ya matumizi. Utafiti huu unahusu Ufaafu wa Mifano ya Matumizi kwenye Kamusi ya Kiswahili Sanifu (TUKI, 2013) katika Kupata Maana ya Kidahizo: Mifano Kutoka Shule za Sekondari. Data za utafiti huu zimekusanywa kwa njia ya hojaji na mahojiano katika shule nane za sekondari wilayani Nyamagana mkoani Mwanza. Aidha, utafiti ulikuwa na malengo yafuatayo: kubainisha uwezo wa wanafunzi wa kutambua mifano ya matumizi iliyomo kwenye KKS (TUKI, 2013), kueleza ni kwa kiasi gani wanafunzi wanaelewa umuhimu wa mifano ya matumizi iliyomo kwenye KKS (TUKI, 2013) na kujadili ufaafu wa mifano ya matumizi katika KKS (TUKI, 2013) kwa wanafunzi na walimu katika shule za sekondari. Utafiti huu umeongozwa na Nadharia ya Maana kama Matumizi. Matokeo ya utafiti yanaonesha kwamba wanafunzi wa shule za sekondari wanaweza kuitambua mifano ya matumizi kwenye kamusi kwa kuangalia namna inavyoandikwa, kusoma utangulizi wa kamusi, kuangalia sentensi zilizo na rangi na kuangalia alama ya wimbi. Vilevile, imebainika kuwa wanafunzi wana uelewa kuhusu mifano ya matumizi kwa kuwa waliweza kueleza umuhimu wa mifano hiyo inavyowasaidia kupata maana ya kidahizo. Pia, data za utafiti huu zimedhihirisha kwamba mifano ya matumizi ni faafu kwa wanafunzi na walimu. Inawasaidia kujifunza maana ya kidahizo, miundo ya sentensi, kuongeza uwezo wa kufikiri, kujifunza semi na kurekebisha makosa mbalimbali ya matumizi ya lugha. Hali kadhalika, walimu huitumia mifano hiyo kufundisha lugha ya Kiswahili kwenye vipengele vya utungaji wa sentensi, maana ya kidahizo na kuondoa utata wa maneno. Kutokana na data za utafiti huu inapendekezwa kuwa matumizi ya kamusi katika shule za sekondari yaboreshwe kwani ni nyenzo muhimu ya kujifunzia lugha.

About Library

The University of Dar es Salaam Library is a vital source of scholarly information that facilitates users to get access to learning and research resources during their studies. It provides access to a wide range of resources in both print and digital formats and conducive reading environment for users, regardless of their physical conditions. All registered users are eligible to access library resources and can borrow print materials from general shelves for a specific period of time.

Useful Links

Koha Staff Login

University Research Repository

WebMail

Aris

Book Study Room

Mara Oral History

Hansard

SOCIAL MEDIA

Instagram

Facebook

Twitter

YouTube

WhatsApp

Ask Librarian

Contact Us

Postal Address
P.O.Box 35092
Dar es Salaam

Call Us: +255 22 2410500/9 Ext. 2165 ; Direct line +255 22 2410241

Fax No:: +255 22 2410241

Email:: directorlibrary@udsm.ac.tz

2025 University of Dar es Salaam - University Of Dar Es Salaam Library
Term of use / Privacy Policy