Repository logo
  • English
  • Català
  • ÄŒeÅ¡tina
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • LatvieÅ¡u
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Log In
    New user? Click here to register. Have you forgotten your password?
Repository logo
    Communities & Collections
    All of DSpace
  • English
  • Català
  • ÄŒeÅ¡tina
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • LatvieÅ¡u
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Log In
    New user? Click here to register. Have you forgotten your password?
  1. Home
  2. Browse by Author

Browsing by Author "Kilapilo, Vianey"

Now showing 1 - 1 of 1
Results Per Page
Sort Options
  • Loading...
    Thumbnail Image
    Item
    Changamoto za kimaana katika kusimbua ujumbe kwenye katuni-mnato-bubu za magazeti ya kiswahili nchini Tanzania.
    (University of Dar es Salaam, 2018) Kilapilo, Vianey
    Matumizi ya katuni-mnato-bubu katika kufikisha ujumbe kwa jamii yanakabiliwa na changamoto mbalimbali za kimaana katika kusimbua ujumbe. Lengo la utafiti lilikuwa ni kuchunguza changamoto za kimaana katika kusimbua ujumbe kwenye katuni-mnato-bubu za magazeti ya Kiswahili nchini Tanzania. Ili kukamilisha utafiti huu, data ilikusanywa kutoka maktabani na uwandani. Mbinu ya uchambuzi matini ilitumika kwa kuwa iliwezesha kukusanywa kwa katuni. Mbinu ya mahojiano ilitumika uwandani na kuwezesha kupatikana kwa data kutoka kwa watoa data asilia. Aidha, nadharia iliyoongoza utafiti huu ni Nadharia ya Alama ya Piece ya mwaka (1904). Misingi yake iliwezesha kubaini changamoto za kimaana zinazotokana na kusimbua ujumbe kwenye katuni-mnato-bubu za magazeti ya Kiswahili. Pia sababu za kutokea kwa changamoto hizo zimebainika na kujadiliwa katika ripoti hii ya utafiti. Kimsingi utafiti umebaini kuwa katuni zina maana na zinabeba ujumbe. Pia, utafiti umebaini kuwa, kuna changamoto za kimaana katika kusimbua ujumbe kwenye katuni. Baadhi ya changamoto hizo ni: kuwapo kwa mkanganyiko wa kimaana, kushindwa kuhusisha matukio katika safu za katuni, kushindwa kusimbua alama ili kujenga maana, na kupotoshwa kwa ujumbe uliokusudiwa na nyingine zilizojadiliwa. Changamoto hizo zinasababishwa na uzoefu wa kimaisha, mtazamo wa mtu au jamii, mila na desturi za jamii, eneo la kijiografia, itikadi zilizopo katika jamii na nyingine zilizojadiliwa. Mwisho, mtafiti anatoa mapendekezo kuwa kuna haja ya kufanya tafiti nyingine kubaini changamoto za kimaana zinazojitokeza katika kusimbua ujumbe kwenye katuni-mnato za aina nyingine na mambo mengine mbalimbali yanayohusu katuni kwa ujumla.

About Library

The University of Dar es Salaam Library is a vital source of scholarly information that facilitates users to get access to learning and research resources during their studies. It provides access to a wide range of resources in both print and digital formats and conducive reading environment for users, regardless of their physical conditions. All registered users are eligible to access library resources and can borrow print materials from general shelves for a specific period of time.

Useful Links

Koha Staff Login

University Research Repository

WebMail

Aris

Book Study Room

Mara Oral History

Hansard

SOCIAL MEDIA

Instagram

Facebook

Twitter

YouTube

WhatsApp

Ask Librarian

Contact Us

Postal Address
P.O.Box 35092
Dar es Salaam

Call Us: +255 22 2410500/9 Ext. 2165 ; Direct line +255 22 2410241

Fax No:: +255 22 2410241

Email:: directorlibrary@udsm.ac.tz

2025 University of Dar es Salaam - University Of Dar Es Salaam Library
Term of use / Privacy Policy