Repository logo
  • English
  • Català
  • ÄŒeÅ¡tina
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • LatvieÅ¡u
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Log In
    New user? Click here to register. Have you forgotten your password?
Repository logo
    Communities & Collections
    All of DSpace
  • English
  • Català
  • ÄŒeÅ¡tina
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • LatvieÅ¡u
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Log In
    New user? Click here to register. Have you forgotten your password?
  1. Home
  2. Browse by Author

Browsing by Author "Kavishe, Agricola Roman"

Now showing 1 - 1 of 1
Results Per Page
Sort Options
  • Loading...
    Thumbnail Image
    Item
    Ujitokezaji wa Falsafa ya Ubuntu katika Riwaya ya Kiswahili; uchaguzi wa adili na nduguze (1952) na siku ya watenzi wote (1968).
    (University of Dar es Salaam, 2019) Kavishe, Agricola Roman
    Utafiti huu umechunguza ujitokezaji wa falsafa ya Ubuntu katika riwaya ya (1952) na Siku ya Watenzi Kiswahili ukijikita katika riwaya ya Adili na Nduguze Wale (1968). Utafiti huu uliongozwa na lengo kuu na malengo mahususi. Lengo kuu la utafiti huu lilikuwa kuchunguza ujitokezaji wa falsafa ya Ubuntu katika riwaya za Adili na Nduguze (1952) na Siku ya Walenzi Wow (1968) za Shaaban Robert.Malengo mahususi yalikuwa matatu nayo ni kubainisha vipengele vya falsafa ya Ubuntu vinavyojitokeza katika riwaya teule za Shaaban Robert, kueleza mbinu anuwai zinazotumika kusawiri vipengele hivyo vya Ubuntu na kufafanua umuhimu wa falsafa ya Ubuntu kisiasa katika riwaya hizo. Nadharia ya Ontolojia ya Kibantu iliyoasisiwa na Tempels (1959) pamoja na wataalamu wengine ndiyo iliyotumika kutikia malengo ya utafiti huu. Ontolojia ya Kibantu ni mtazamo wa jamii ya Wabantu kuhusu maisha, kuwapo kwa mwanadamu na ulimwengu kwa ujumla. Utafiti huu ulikuwa wa maktabani, mbinu za ukusanyaji wa data maktabani ulifanywa kwa kusoma maandiko na machapisho mbalimbali kwenye magazeti, majarida, vitabu vinavyohusiana na mada husika, pamoja na makala zilizo mtandaoni. Mtafiti alikusanya data zinazohusiana na falsafa ya Ubuntu kutoka katika riwaya zilizoteuliwa na kuzifafanua, kisha kubaini mbinu zilizotumika kusawiri falsafa ya Ubuntu katika riwaya hizo na umuhimu wa falsafa hiyo kisiasa. Tasinifu mbalimbali zilizozungumzia falsafa ya Ubuntu kwa namna mbalimbali zilitumika kupata taarifa. Vipengele vilivyojitokeza ndivyo vilivyojenga data kuu iliyofanyiwa uchambuzi na uhakiki. Matokeo ya data katika uchambuzi yalibainisha kwamba vipengele vya falsafa ya Ubuntu vinavyojitokeza katika riwaya hizo ni: utu, kazi, wema, busara, hekima na haki na usawa. Vipengele vingine ni ndoa, ukarimu, upendo, malezi, huruma halikadhalika umoja na ushirikiano. Mbinu mbalimbali zilizotumika kusawiri vipengele hivyo ni methali, barua, nyimbo, kilio, kicheko na lugha ya watoto. Ilibainika kwamba vipengele vya falsafa ya Ubuntu vina umuhimu mkubwa kisiasa katika riwaya teule. Umuhimu huo ni pamoja na kujenga uongozi bora, kusaidia raia wenye shida, kupigania haki na usawa, kujali utu wa raia, na kuwa mwema kwa raia. Aidha, utafiti umebaini kuwa mwandishi Shaaban Robert katika riwaya zake zilizotafitiwa amesawiri vipengele mbalimbali vya falsafa ya Ubuntu ambavyo tunaamini ndiyo falsafa iliyomkuza pamoja na jamii yake. Hii inatueleimisha zaidi kuhusu falsafa ya Shaaban Robert kuwa hakuathiriwa to na falsafa ya Kimagharibi na mtazamo wa dini ya Kiislamu. Utafiti huu umetoa muongozo kwa waandishi na wahakiki wa kazi za fasihi kuhusu ujitokezaji wa falsafa ya Ubuntu na inavyosawiri maisha ya waandishi na jamii kwa ujumla.

About Library

The University of Dar es Salaam Library is a vital source of scholarly information that facilitates users to get access to learning and research resources during their studies. It provides access to a wide range of resources in both print and digital formats and conducive reading environment for users, regardless of their physical conditions. All registered users are eligible to access library resources and can borrow print materials from general shelves for a specific period of time.

Useful Links

Koha Staff Login

University Research Repository

WebMail

Aris

Book Study Room

Mara Oral History

Hansard

SOCIAL MEDIA

Instagram

Facebook

Twitter

YouTube

WhatsApp

Ask Librarian

Contact Us

Postal Address
P.O.Box 35092
Dar es Salaam

Call Us: +255 22 2410500/9 Ext. 2165 ; Direct line +255 22 2410241

Fax No:: +255 22 2410241

Email:: directorlibrary@udsm.ac.tz

2025 University of Dar es Salaam - University Of Dar Es Salaam Library
Term of use / Privacy Policy