Repository logo
  • English
  • Català
  • ÄŒeÅ¡tina
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • LatvieÅ¡u
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Log In
    New user? Click here to register. Have you forgotten your password?
Repository logo
    Communities & Collections
    All of DSpace
  • English
  • Català
  • ÄŒeÅ¡tina
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • LatvieÅ¡u
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Log In
    New user? Click here to register. Have you forgotten your password?
  1. Home
  2. Browse by Author

Browsing by Author "Katoto, Zuhura Jumla"

Now showing 1 - 1 of 1
Results Per Page
Sort Options
  • Loading...
    Thumbnail Image
    Item
    Usawiri wa falsafa ya kiafrika katika unyago wa jamii ya wamakonde: uchunguzi wa nyimbo za unyago wa Chiputu.
    (University of Dar es Salaam, 2016) Katoto, Zuhura Jumla
    Utafiti huu unahusu Usawiri wa Falsafa ya Kiafrika katika Unyago wa Jamii ya Wamakonde: Uchunguzi wa Nyimbo za Unyago wa Chiputu. Tatizo la utafiti lilitokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia yalivyobadilisha jamiihadi utanzu huu ukaanza kuonekana kuwaumepitwa na wakati na hauna maana. Utafiti huu ulifanywa ili kuonyesha kuwa unyago bado una dhima. Tulikusudia kuchunguza dhima mojawapo ya unyago wa jamii ya Wamakonde, ya kusawiri falsafa ya Kiafrika. Kwa hiyo, utafiti huu ulikuwa na malengo yakufafanua utendaji wa nyimbo katika unyago wa Wamakonde, kubainisha falsafa ya Kiafrika inayosawiriwa na nyimbo za unyago wa Chiputu wa Wamakonde, na mwisho kueleza dhima ya usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika nyimbo za unyago wa Wamakonde.Ili kufanya hayo, utafiti huu ulihusisha data zilizokusanywa uwandani kwa njia mbalimbali zinazojumuisha uchambuzi matini, ushuhudiaji wa kushiriki namahojiano huru. Aidha, utafiti wa maktabani ulisaidia kukamilisha malengo ya utafiti huu ambapo nyaraka mbalimbali kama vitabu, majarida vilidurusiwa. Katika uchambuzi na ufasiri wa data, nadharia ya Kijamii (Sosholojia ya Fasihi) ilitusaidia kuchunguza uhusiano wa unyago na imani za jamii inayohusika. Pia, nadharia ya Ontolojia ya Kibantu ilitumikakubainisha jinsi masuala yanayosawiriwa katika nyimbo za unyago wa Wamakonde.Matokeo ya utafiti yalidhihirisha kuwa, kuna aina tatu za nyimbo za unyago wa chiputu kwa Wamakonde na kila kipindi kina utendaji wake.Nyimbo ambazo huimbwa kwa madhumuni ya kufundishia wari mambo mbalimbali na ambazo hubeba falsafa ya Kiafrika.Miongoni mwa falsafa hizo ni falsafa kuwa kifo si mwisho wakuwapo;falsafa kuhusu mizimu na nguvuzao katikakuwasaidia wanadamu; falsafa kuhusu Mungu na uwezo wake, na; falsafa kuhusu nafasi ya mwanamke na mwanamume katika jamii. Falsafa nyingine nikuhusu uzazi na malezi; falsafa kuhusu imani za uchawi, uganga na sihiri; falsafa kuhusu utu;na falsafa kuhusu heshima kwa wakubwa. Pia, imebainika kuwa usawiri huu wa falsafa ya Kiafrika katika unyago wa chiputu una dhima,miongoni mwa dhima hizo ni kurithisha imani mbalimbali kwa kizazi kipya; kutoa mafunzo mbalimbali kwa vijana; kuifanya jamii ya Wamakonde kufanana na jamii nyingine za Kiafrika; kuendeleza umoja, amani na utangamano katika jamii ya Wamakonde, na; kuleta maendeleo ya kiuchumi na kijamii katika jamii ya Wamakonde. Hata hivyo, inapendekezwa kufanyika kwa tafiti zaidikuhusu usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika vipengele vingine vya unyago kama vile hadithi, maigizo na misemo, ili kuweza kutoa majumuisho kuhusu usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika unyago wa Wamakonde. Aidha, tafiti zaidi zinahitajika ili kulinganisha usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika nyimbo za unyago wa jamii ya Wamakonde na unyago wa jamii nyingine.

About Library

The University of Dar es Salaam Library is a vital source of scholarly information that facilitates users to get access to learning and research resources during their studies. It provides access to a wide range of resources in both print and digital formats and conducive reading environment for users, regardless of their physical conditions. All registered users are eligible to access library resources and can borrow print materials from general shelves for a specific period of time.

Useful Links

Koha Staff Login

University Research Repository

WebMail

Aris

Book Study Room

Mara Oral History

Hansard

SOCIAL MEDIA

Instagram

Facebook

Twitter

YouTube

WhatsApp

Ask Librarian

Contact Us

Postal Address
P.O.Box 35092
Dar es Salaam

Call Us: +255 22 2410500/9 Ext. 2165 ; Direct line +255 22 2410241

Fax No:: +255 22 2410241

Email:: directorlibrary@udsm.ac.tz

2025 University of Dar es Salaam - University Of Dar Es Salaam Library
Term of use / Privacy Policy