Repository logo
  • English
  • Català
  • ÄŒeÅ¡tina
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • LatvieÅ¡u
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Log In
    New user? Click here to register. Have you forgotten your password?
Repository logo
    Communities & Collections
    All of DSpace
  • English
  • Català
  • ÄŒeÅ¡tina
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • LatvieÅ¡u
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Log In
    New user? Click here to register. Have you forgotten your password?
  1. Home
  2. Browse by Author

Browsing by Author "Elias, Lustica"

Now showing 1 - 1 of 1
Results Per Page
Sort Options
  • Loading...
    Thumbnail Image
    Item
    Mfuatano wa mofimu ambatizi katika kitenzi cha Kiluguru
    (University of Dar es Salaam, 2016) Elias, Lustica
    Utafiti huu umechunguza mfuatano wa mofimu ambatizi katika kitenzi cha Kiluguru. Malengo ya utafiti huu ni pamoja na kubaini aina za mofimu ambatizi na dhima zake katika kitenzi cha Kiluguru, kufafanua mfuatano wa mofimu hizo na kueleza kanuni zinazojitokeza wakati wa uambatizi. Sababu ya kuchunguza kipengele hiki ni kutoa mchango wa uelewa wetu wa suala la uambatizi katika lugha za jamii ya kibantu ikiwemo lugha ya Kiluguru. Uambatizi ni dhana inayojitokeza sana katika lugha za kibantu lakini udadavuzi wake huwa na changamoto za pekee katika lugha husika. Kuna kuachana na kutofautiana kwingi katika taratibu za uchambuzi. Na katika lugha hii ya Kiluguru suala hili halijafanyiwa utafiti wa kutosha. Ili kufikia malengo hayo, ilikusanywa data ya utafiti toka uwandani ambako vitenzi mbalimbali vyenye ukomo viliteuliwa na kuchambuliwa. Ukusanyaji wa data ulifanyika katika vijiji viwili, yaani Nyandira katika wilaya ya Mvomero na Kibangile katika wilaya ya Morogoro vijijini, mkoani Morogoro, Tanzania. Taarifa zilikusanywa kwa njia ya mahojiano na ushuhudiaji. Mahojihano yalitumika sambamba na dodoso. Aidha utafiti huu uliongozwa na nadharia ya Mofolojia Leksika ya Kiparsky (1982) ambayo msingi wake unadai kuwa maneno yanaundwa na vipande vidogo vidogo ambavyo hupangwa katika ngazi na kuonesha uhusiano wa kanuni zinazojenga maumbo ya kimofolojia na kanuni zinazodhibiti namna maumbo haya yanavyotamkwa. Matokeo ya utafiti yameonesha uwepo wa mofimu nyingi ambatizi katika Kiluguru kama vile mofimu za nafsi, njeo, ukanushi, yambwa, urejeshi na hali. Imebainika pia kuwa mifuatano kubalifu ya mofimu ambatizi katika vitenzi vya Kiluguru si huru bali hutawaliwa na kanuni mahususi; imebainika pia kuwa mifuatano hiyo kisintakisia huukilia dhima tofauti tofauti za mofimu husika. Pia utafiti umebaini kuwepo kwa kanuni mbalimbali zinazojitokeza wakati wa uambatizi kama vile kanuni ya udondoshaji wa irabu, uyeyushaji, usimilishaji wa nazali na muungano au mvutano wa irabu.

About Library

The University of Dar es Salaam Library is a vital source of scholarly information that facilitates users to get access to learning and research resources during their studies. It provides access to a wide range of resources in both print and digital formats and conducive reading environment for users, regardless of their physical conditions. All registered users are eligible to access library resources and can borrow print materials from general shelves for a specific period of time.

Useful Links

Koha Staff Login

University Research Repository

WebMail

Aris

Book Study Room

Mara Oral History

Hansard

SOCIAL MEDIA

Instagram

Facebook

Twitter

YouTube

WhatsApp

Ask Librarian

Contact Us

Postal Address
P.O.Box 35092
Dar es Salaam

Call Us: +255 22 2410500/9 Ext. 2165 ; Direct line +255 22 2410241

Fax No:: +255 22 2410241

Email:: directorlibrary@udsm.ac.tz

2025 University of Dar es Salaam - University Of Dar Es Salaam Library
Term of use / Privacy Policy