Repository logo
  • English
  • العربية
  • বাংলা
  • Català
  • Čeština
  • Deutsch
  • Ελληνικά
  • Español
  • Suomi
  • Français
  • Gàidhlig
  • ગુજરાતી
  • हिंदी
  • Magyar
  • Italiano
  • Қазақ
  • Latviešu
  • मराठी
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Русский
  • Srpski (lat)
  • Српски
  • Svenska
  • Türkçe
  • Yкраї́нська
  • Tiếng Việt
  • Log In
    New user? Click here to register.Have you forgotten your password?
Repository logo
  • Communities & Collections
  • View all
  • English
  • العربية
  • বাংলা
  • Català
  • Čeština
  • Deutsch
  • Ελληνικά
  • Español
  • Suomi
  • Français
  • Gàidhlig
  • ગુજરાતી
  • हिंदी
  • Magyar
  • Italiano
  • Қазақ
  • Latviešu
  • मराठी
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Русский
  • Srpski (lat)
  • Српски
  • Svenska
  • Türkçe
  • Yкраї́нська
  • Tiếng Việt
  • Log In
    New user? Click here to register.Have you forgotten your password?
  1. Home
  2. Browse by Author

Browsing by Author "Sovu, Yahya Ahmad"

Now showing 1 - 1 of 1
Results Per Page
Sort Options
  • Loading...
    Thumbnail Image
    Item
    Uchanganuzi wa mbinu za kisarufi na kibalagha katika vilongo teule vya kampeni za uchaguzi wa mwaka 2015, nchini Tanzania
    (University of Dar es Salaam, 2020) Sovu, Yahya Ahmad
    Utafiti huu ulilenga kuchunguza lugha ya kisiasa, hususani katika kipindi cha kampeni za uchaguzi wa 2015 nchini Tanzania. Hoja kuu ikiwa ni kuchambua kwa undani mbinu za wanasiasa na nduni anuwai wanazozitumia katika mikutano ya kampeni za uchaguzi. Ili kutimiza hoja hii utafiti ulilenga hasa kubaini nduni za kisarufi na kibalagha katika vilongo teule vya hotuba za kampeni za uchaguzi za mwaka 2015, kuchunguza dhima zake katika kampeni za uchaguzi na kupambanua iwapo mbinu hizo zina athari chanya na hasi kwa hadhira. Data za utafiti zilikusanywa maktabani na uwandani kwa kutumia mbinu ya uchambuzi wa nyaraka, usikilizaji wa hotuba, usomaji wa maandiko, usaili, na hojaji. Mkabala wa kitaamuli, na wa kiidadi kwa kiasi kidogo ilitumika kuchambua data zote. Mkabala wa Uchanganuzi Tunduizi Kilongo pamoja na Nadharia ya Balagha zimetumika katika utafiti huu. Matokeo ya utafiti yameonesha kwamba, hali ya ukinzani baina ya kambi za UKAWA na CCM imejidhihirisha katika lugha za kampeni kupitia mbinu za uteuzi wa maneno, vijenzi vya sarufi na tamathali za kibalagha. Matokeo yameonesha zaidi kuwa, kauli zenye kutweza afya ya wagombea, kejeli, kashfa na vitisho zilitumiwa. Pia, kauli zenye kuhimiza amani, mshikamano, kufanya kazi kwa bidii zilisikika. Matumizi ya nafsi ya kwanza "ni-", lugha za mitaani, takriri, jazanda, chuku, misimu, methali, mbazi za kidini, sitiari na vionjo anuwai vya lugha vilifumbatwa iii kufikia malengo hayo. Vilevile, matokeo yameonesha kwamba, mbinu hizi zina dhima ya urembeshaji, ufafanuaji, usisimuaji, uthibitishaji na hata ujikurubishaji kwa hadhira. Pia, imebainika kwamba, mbinu za kisarufi na kibalagha zimeibua athari chanya za kuburudisha, kuhimiza, kuzindua, kujenga matumaini na athari hasi zinazochochea ubaguzi, udhalilishaji, na kujenga uhasama miongoni mwa wanajamii.Utafiti huu umechangia katika taaluma ya uchanganuzi vilongo. Mchango mahususi umejikita katika kubaini sifa za lugha ya kampeni za kisiasa kama rejista maalumu. utafiti huu unapendekeza wazungumzaji katika hotuba za kampeni za uchaguzi wazingatie matumizi mazuri ya lugha yenye kujenga umoja na mshikamno, pia waache kuendeleza matumizi ya lugha zisizo za staha, matusi na kejeli ambazo zinaweza kuchochea migogoro miongoni mwa hadhira wanazozihutubia.

About Library

The University of Dar es Salaam Library is a vital source of scholarly information that facilitates users to get access to learning and research resources during their studies. It provides access to a wide range of resources in both print and digital formats and conducive reading environment for users, regardless of their physical conditions. All registered users are eligible to access library resources and can borrow print materials from general shelves for a specific period of time.

Useful Links

Koha Staff Login

University Research Repository

WebMail

Aris

Book Study Room

Mara Oral History

Hansard

SOCIAL MEDIA

Instagram

Facebook

Twitter

YouTube

WhatsApp

Ask Librarian

Contact Us

Postal Address
P.O.Box 35092
Dar es Salaam

Call Us: +255 22 2410500/9 Ext. 2165 ; Direct line +255 22 2410241

Fax No:: +255 22 2410241

Email:: directorlibrary@udsm.ac.tz

2025 University of Dar es Salaam - University Of Dar Es Salaam Library
Term of use / Privacy Policy