Repository logo
  • English
  • Català
  • ÄŒeÅ¡tina
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • LatvieÅ¡u
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Log In
    New user? Click here to register. Have you forgotten your password?
Repository logo
    Communities & Collections
    All of DSpace
  • English
  • Català
  • ÄŒeÅ¡tina
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • LatvieÅ¡u
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Log In
    New user? Click here to register. Have you forgotten your password?
  1. Home
  2. Browse by Author

Browsing by Author "Sigimba, Jimson Nasson"

Now showing 1 - 1 of 1
Results Per Page
Sort Options
  • No Thumbnail Available
    Item
    Uainishaji wa ngeli za nomino za kikinga: mtazamo wa kimofolojia na kisemantiki Jimson Nasson Sigimba
    (University of Dar es Salaam, 2014) Sigimba, Jimson Nasson
    Malengo ya utafiti huu yalikuwa ni kuziainisha ngeli za nomino za Kikinga kwa mtazamo wa kimofolojia na kisemantiki na kujua idadi yake. Aidha, ufafanuzi wa mtawanyiko wa nomino zenye asili moja kisemantiki na dhima zinazojitokeza katika viambishi ngeli vya nomino za Kikinga umeshughulikiwa. Utafiti huu umefanyika katika vijiji vya Ikonda, Iwawa, Tandala na Bulongwa Wilayani Makete ambamo watafitiwa 32 kutoka vijiji hivyo waliteuliwa. Njia za ukusanyaji wa data zilizotumika ni hojaji, mahojiano na ushuhudiaji. Nadharia ya Mofolojia Asilia iliongoza utafiti huu ili kuweza kufafanua dhima mbalimbali zinazojitokeza katika viambishi ngeli vya nomino za Kikinga. Utafiti huu umegawanyika katika sura tano. Sura ya Kwanza inahusu maelezo yahusuyo eneo la utafiti, usuli wa tatizo, mfumo wa sauti za Kikinga, historia ya Wakinga, michakato ya kimofolojia, malengo ya utafiti, maswali na umuhimu wa utafiti na msingi wa nadharia. Katika Sura ya Pili, machapisho mbalimbali yaliyohusu uainishaji wa ngeli katika lugha za Kibantu yamepitiwa ili kuweza kujua namna ya kutafiti mada husika kwa kutumia mbinu za wataalamu waliotangulia. Sura ya Tatu inahusu mbinu za utafiti zilizotumika katika ukusanyaji wa data. Uchanganuzi na uwasilishaji wa data iliyokusanywa uwandani umefafanuliwa katika Sura ya Nne. Katika sura hii ngeli za nomino za Kikinga zimeainishwa kwa kutumia kigezo cha kimofolojia na kisemantiki. Utafiti huu umebaini pia kuwa ngeli za Kikinga huanza na Irabu Tangulizi (IT) kisha kufuatiwa na Kiambishi Ngeli (Kng) na Shina (Sh). Kiambishi ngeli cha nomino (Kng) ndicho kilichotumika kuainisha ngeli za nomino za Kikinga na sio irabu tangulizi (IT). Sura ya Tano imeelezea matokeo ya utafiti, mapendekezo ya tafiti fuatishi na hitimisho. Utafiti huu umebaini kuwa lugha ya Kikinga ina ngeli za nomino 19 kwa mtazamo wa kimofolojia. Pia, imeonekana kuna mtawanyiko wa nomino za Kikinga katika ngeli tofauti tofauti isipokuwa ngeli inayohusu watu, nomino za mkopo, vitu dhahania, vitu visivyohesabika, zenye dhima ya udogo na mahali zinapoainishwa kimofolojia na kisemantiki. Zaidi ya hayo imebainika kuwa viambishi ngeli vya nomino za Kikinga vinaweza kubeba dhima ya kuonesha umoja, wingi, uzuri, ubaya, udogo na ukubwa.

About Library

The University of Dar es Salaam Library is a vital source of scholarly information that facilitates users to get access to learning and research resources during their studies. It provides access to a wide range of resources in both print and digital formats and conducive reading environment for users, regardless of their physical conditions. All registered users are eligible to access library resources and can borrow print materials from general shelves for a specific period of time.

Useful Links

Koha Staff Login

University Research Repository

WebMail

Aris

Book Study Room

Mara Oral History

Hansard

SOCIAL MEDIA

Instagram

Facebook

Twitter

YouTube

WhatsApp

Ask Librarian

Contact Us

Postal Address
P.O.Box 35092
Dar es Salaam

Call Us: +255 22 2410500/9 Ext. 2165 ; Direct line +255 22 2410241

Fax No:: +255 22 2410241

Email:: directorlibrary@udsm.ac.tz

2025 University of Dar es Salaam - University Of Dar Es Salaam Library
Term of use / Privacy Policy