Repository logo
  • English
  • Català
  • ÄŒeÅ¡tina
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • LatvieÅ¡u
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Log In
    New user? Click here to register. Have you forgotten your password?
Repository logo
    Communities & Collections
    All of DSpace
  • English
  • Català
  • ÄŒeÅ¡tina
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • LatvieÅ¡u
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Log In
    New user? Click here to register. Have you forgotten your password?
  1. Home
  2. Browse by Author

Browsing by Author "Nnileka, Sharifa Mauridi"

Now showing 1 - 1 of 1
Results Per Page
Sort Options
  • Loading...
    Thumbnail Image
    Item
    Matumizi ya nadharia ya korasi katika uhakiki wa hadithi fupi: mifano kutoka mayai waziri wa maradhi na hadithi nyingine
    (University of Dar es Salaam, 2019) Nnileka, Sharifa Mauridi
    Utafiti huu unahusu matumizi ya Nadharia ya 〖Korasi〗^1 katika uhakiki wa hadithi fupi: Mifano iliyotumiwa imetolewa kutoka Mayai Waziri wa Maradhi na Hadithi Nyingine. Utafiti huu uliongozwa na malengo mahususi matatu ambayo ni kubainisha vipengele vya Nadharia ya Korasi katika hadithi fupi mifano kutoka Mayai Waziri wa Maradhi na Hadithi Nyingine. Kubainisha matumizi mbalimbali ya vipengele vya Nadharia ya Korasi katika hadithi fupi za Mayai Waziri wa Maradhi na Hadithi Nyingine na kujadili umuhimu wa Nadharia ya Korasi katika uhakiki wa hadithi fupi. Utafiti huu ulipitia machapisho mbalimbali hasa yanayohusu uhakiki wa kazi za fasihi, hadithi fupi, Korasi na Nadharia ya Korasi. Korasi ni matendo, fikra au maneno ya kisanaa yanayojitokeza katika kazi ya sanaa ambayo humfanya msomaji au msikilizaji wa kazi ya sanaa kufikiria undani wa naneno, fikra au matendo hayo tofauti na kama maneno, fikra au matendo hayo yasingalijitokeza kwa namna yalivyojitokeza Utafiti huu uliongozwa na Nadharia ya Korasi. Misingi na mihimili ya Nadharia ya Korasi iliwezesha kubaini matendo, maneno na fikra za kisanaa zinazojitokeza katika kila hadithi fupi kutoka Mayai Waziri wa Maradhi na Hadithi Nyingine na hivyo kupata data za utafiti huu Aidha, mihimili ya Nadharia ya Korasi na hivyo kuzitafsiri kulingana na ujitokezaji wa korasi husika. Utafiti huu ulifanyika maktabani ambapo ukusanyaji wa data ulitumia mbinu ya usomaji makini na upitiaji wa machapisho. Matokeo ya utafiti huu yameonesha kwamba, Nadharia ya Korasi ni faafu katika uhakiki wa hadithi fupi. Katika hadithi fupi korasi imeweza kujitokeza kama tukio la kijamii, kama mhusika, kama sauti, kama kimya, kama ukengeushi, kama dhamira, kama muundo, kama mtindo, kama wimbo, kama imani, kama miviga na kama usimulizi. Umuhimu wa Nadharia ya Korasi uliobainika katika utafiti huu ni pamoja na kuwezesha kuchunguza ubunifu wa mwandishi, kuibua masuala ambayo hayajadiliwi kwa uwazi katika jamii, kukuza udadisi, kuondoa dhana ya kimapokeo inayoeleza kuwa kuhakiki fasihi ni lazima kutenganisha fani na maudhui, na kuhakiki matendo yasiyokuwa na maneno.

About Library

The University of Dar es Salaam Library is a vital source of scholarly information that facilitates users to get access to learning and research resources during their studies. It provides access to a wide range of resources in both print and digital formats and conducive reading environment for users, regardless of their physical conditions. All registered users are eligible to access library resources and can borrow print materials from general shelves for a specific period of time.

Useful Links

Koha Staff Login

University Research Repository

WebMail

Aris

Book Study Room

Mara Oral History

Hansard

SOCIAL MEDIA

Instagram

Facebook

Twitter

YouTube

WhatsApp

Ask Librarian

Contact Us

Postal Address
P.O.Box 35092
Dar es Salaam

Call Us: +255 22 2410500/9 Ext. 2165 ; Direct line +255 22 2410241

Fax No:: +255 22 2410241

Email:: directorlibrary@udsm.ac.tz

2025 University of Dar es Salaam - University Of Dar Es Salaam Library
Term of use / Privacy Policy