Repository logo
  • English
  • Català
  • ÄŒeÅ¡tina
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • LatvieÅ¡u
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Log In
    New user? Click here to register. Have you forgotten your password?
Repository logo
    Communities & Collections
    All of DSpace
  • English
  • Català
  • ÄŒeÅ¡tina
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • LatvieÅ¡u
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Log In
    New user? Click here to register. Have you forgotten your password?
  1. Home
  2. Browse by Author

Browsing by Author "Mwalwisi, Anna Benjamini"

Now showing 1 - 1 of 1
Results Per Page
Sort Options
  • Loading...
    Thumbnail Image
    Item
    Uzingativu wa kanuni ya uhusiano katika mahubiri ya dini ya kikristo
    (University of Dar es Salaam, 2017) Mwalwisi, Anna Benjamini
    Tasinifu hii imejadili ‘Uzingativu wa Kanuni ya Uhusiano Katika Mahubiri ya Dini ya Kikristo’. Hivyo, mahubiri manne tofauti yamechunguzwa. Aidha, kutokana na malengo ya utafiti huu, tasinifu imejadili namna mahubiri hayo yanavyoizingatia kanuni ya uhusiano kwa kuviangalia vipengele mbalimbali vilivyohusianishwa na mahubiri hayo. Vipengele hivyo ni kama vile; uhusiano wa lugha ya mahubiri na wasikilizaji, uhusiano wa mahubiri na mada, kichwa, mifano, ukristo, wakati, na kadhalika. Utafiti huu umefanywa ndani ya wilaya ya Mbeya mjini na kuhusisha waumini wa dini ya Kikristo wenye umri na vyeo mbalimbali vya kihuduma yaani wachungaji, wazee wa kanisa n.k. kutoka madhehebu tofautitofauti walihojiwa. Utafiti huu umetumia Nadharia ya Umanilizi pamoja na Nadharia ya Mwitiko wa Msomaji/Msikilizaji. Nadharia ya Umanilizi ilitumiwa kubaini uvunjifu wa kanuni ya uhusiano na madhara yake katika mahubiri. Wakati, Nadharia ya Mwitiko wa Msomaji/Msikilizaji ilitumiwa kubaini mitazamo ya watafitiwa/wasikilizaji wa mahubiri juu ya uhusiano wa mahubiri na vipengele mbalimbali vilivyohusishwa nayo. Mwisho, tasinifu hii imethibitisha kuwa mahubiri ya dini yaliyotafitiwa yana uzingativu wa kanuni ya uhusiano kwa kiasi kikubwa na pia yana uvunjifu wa kanuni hiyo kwa kiasi kidogo. Uzingativu huo umetokana na lugha ya mahubiri kuwazingatia wasikilizaji, mahubiri kuizingatia jamii husika, mahubiri kuhubiriwa kwa mitindo ya ufafanuzi wa mada, nukuu ya mada, usimulizi wa mada n.k. Aidha, uvunjifu wa kanuni ya uhusiano pia umejitokeza katika mahubiri hayo na kusababisha madhara mbalimbali, kama vile: maana ya mahubiri kuwa tata kutokana na dhahania mbalimbali juu ya maana ya mahubiri hayo, hivyo mahubiri kuwa na uziada dufu wa maana; maana za mahubiri kupungua au kuongezeka kutokana na kuibuka kwa dhahania mbalimbali juu ya maana za mahubiri; kwa mfano, uvunjifu wa uhusiano wa mahubiri na mada ya mahubiri kulingana na muktadha wa dini kumeibua maana mbadala za mahubiri kutoka kwa wachungaji waliotafitiwa.

About Library

The University of Dar es Salaam Library is a vital source of scholarly information that facilitates users to get access to learning and research resources during their studies. It provides access to a wide range of resources in both print and digital formats and conducive reading environment for users, regardless of their physical conditions. All registered users are eligible to access library resources and can borrow print materials from general shelves for a specific period of time.

Useful Links

Koha Staff Login

University Research Repository

WebMail

Aris

Book Study Room

Mara Oral History

Hansard

SOCIAL MEDIA

Instagram

Facebook

Twitter

YouTube

WhatsApp

Ask Librarian

Contact Us

Postal Address
P.O.Box 35092
Dar es Salaam

Call Us: +255 22 2410500/9 Ext. 2165 ; Direct line +255 22 2410241

Fax No:: +255 22 2410241

Email:: directorlibrary@udsm.ac.tz

2025 University of Dar es Salaam - University Of Dar Es Salaam Library
Term of use / Privacy Policy