Repository logo
  • English
  • Català
  • Čeština
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • Latviešu
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Log In
    New user? Click here to register. Have you forgotten your password?
Repository logo
    Communities & Collections
    All of DSpace
  • English
  • Català
  • Čeština
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • Latviešu
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Log In
    New user? Click here to register. Have you forgotten your password?
  1. Home
  2. Browse by Author

Browsing by Author "Mahenge, Elizabeth Godwin"

Now showing 1 - 2 of 2
Results Per Page
Sort Options
  • Loading...
    Thumbnail Image
    Item
    Uumbaji Wa Ualbino Katika Fasihi Ya Kiswahili; Uchambuzi Wa Kazi Teule
    (Chuo Kikuu cha Dar es salaam, 2019) Mahenge, Elizabeth Godwin
    Utafiti huu ulihusu uchambuzi wa kazi teule katika fasihi ya Kiswahili ili kuona namna uumbaji wa albino unavyofanyika. Utafiti ulikuwa na malengo mahsusi manne ambayo ni kubainisha imani zinazoumba ualbino katika kazi teule za fasihi ya Kiswahili; kuelezea dhima ya msimulizi zinazotumiwa kuumba ualbino katika kazi teule.Utafiti ulihusisha kazi nane za fasihi ya Kiswahili ambazo ni Takadini, Nje Ndani, Zindera, Baba Ne-Musa “Mimi Albino”, Wimbo wangu Albino”, “Albino” na “Mauaji ya Albino,” Mbinu ya uchambuzi wa nyaraka ilitumika ili kupata matokeo ya utafiti huu. Mbinu hii ya uchambuzi wa nyaraka ilitumika ili kupata matokeo ya utafiti huu. Mbinu hii ya uchambuzi iliongozwa na Nadharia ya Naratolojia. Nadharia hii inahusika kuchunguza namna usimulizi unavyofanywa katika simulizi.Utafiti unafuata mkabala wa Bal ambao unaona kuna usimulizi kaitika kila kitu. Data zilipatikana baada ya kusoma kwa kina kazi teule pamoja na kufanya mahojiano kwa ajili ya utafiti wa awali wa utafiti huu. Mkabala uliotumika katika uchambuzi wa data ni wa kitaamuli ambao ni wa kimaelezo na uliwezesha kupatikana kwa matokeo ya utafiti huu. Kwanza , utafiti umebaini kuwa kuna imani mbalimbali zinazoelezea asili ya kuzaliwa motto mwenye ualbino. Imani hizi zinatokana na visasili vilivyopo katika jamii.Pili, utafiti umebaini kuwa , msimulizi anatumia tamathali za usemi ili kuumba ualbino kiubaguzi na kiunyanyapaa kwa upande mmoja; na pia anatumia tamathali za usemi ili kuumba ualbino kiujumuishwaji kwa pande mwingine.Tatu, utafiti umebaini kuwa msimulizi anajititokeza kwa dhima ynne ambazo ni kusimulia kuwasiliana, kukosoa na kutekeleza itikadi. Katika dhima hizi, msimulizi anawezakuwa hai (akishiriki katika kusimulia) au tuli( akijenga kusimulia), Nne, utafiti umebaini kuwa , sauti za usimulizi zinatumika kwa makusudi maalum ambayo ni ama kuunga knono jambo Fulani au kulipinga. Matumizi ya nafi ya kwanza nay a pili yanaonesha kuunga mkono jambo; wakati matumizi ya nafsi ya tatu yanaonesha kulipinga. Mapendekezo yanayotolea na utafiti huu ni kufanya utafiti mwingine katika kumbo mahususi za fasihi ili kuona namna ualbino kwa umahususi na ulemavu kwa ujumla unavyoumbwa katika kumbo hizo Vilevile utafiti unapendekeza nadharia ya Naratolojia itumiwe zaidi na wachambuzi wa kazi za kifasihi kwa kuwa inamwezesha mchambuzi kuufahamu uhalisia wa simulizi kupitia nafsi mahususi zinazotumika katika kusimulia.Nadharia hii iko karibu na uhalisia.
  • Loading...
    Thumbnail Image
    Item
    Uumbaji wa ualbino katika fasihi ya kiswahili: uchambuzi wa kazi teule
    (University of Dar es Salaam, 2019) Mahenge, Elizabeth Godwin
    Utafiti huu ulihusu uchambuzi wa kazi teule katika fasihi ya kiswahili ili kuona namna uumbaji wa ualbino unavyofanyika. Utafiti ulikuwa na malengo mahususi manne ambayo ni: kubainisha imani zinazoumba ualbino katika kazi teule za fasihi ya Kiswahili; kuchambua jinsi lugha inavyoumba ualbino katika kazi teule za fasihi ya Kiswahili; kuelezea dhima ya msimulizi anayesimulia hadithi ya ualbino katika kazi teule; na kujadili sauti za usimulizi zinazotumiwa kuumba ualbino katika kazi teule. Utafiti ulihusisha kazi nane za fasihi ya Kiswahili ambazo ni: Takadini, Nje Ndani, Zindera, Baba Ne-Musa!,"Mimi Albino", "Wimbo Wangu Albino" "Albino", na "Mauaji ya Albino". Mbinu ya uchambuzi wa nyaraka ilitumika ili kupata matokeo ya utafiti huu. Mbinu hii ya uchambuzi iliongozwa na Nadharia ya Naratolojia. Nadharia hii inahusika kuchunguza namna usimulizi unavyofanywa katika simulizi. Utafiti unafuata mkabala wa Bal ambao unaona kuna usimulizi katika kila kitu. Data zilipatikana baada ya kusoma kwa kina kazi teule pamoja na kufanya mahojiano kwa ajili ya utafiti wa awali wa utafiti huu. Mkabala uliotumika katika uchambuzi wa data ni wa kitaamuli ambao ni wa kimaelezo na uliwezesha kupatikana kwa matokeo ya utafiti huu. Kwanza, utafiti umebaini kuwa kuna imani mbalimbali zinazoelezea asili ya kuzaliwa mtoto mwenye ualbino. Imani hizi zinatokana na visasili vilivyopo katika jamii. Pili, utafiti umebaini kuwa, msimulizi anatumia tamathali za usemi ili kuumba ualbino kiubaguzi na kiunyanyapaa kwa upande mmoja; na pia anatumia tamathali za usemi ili kuumba ualbino kiujumuishwaji kwa upande mwingine. Tatli, utafiti umebaini kuwa msimulizi anajitokeza kwa dhima nne ambazo ni kusimulia, kuwasiliana, kukosoa na kutekeleza itikadi. Katika dhima hizi, msimulizi anaweza kuwa hai (akishiriki katika kusimulia) au tuli (akijitenga kusimulia). Nne, utafiti umebaini kuwa, sauti za usimulizi zinatumika kwa makusudi maalumu ambayo ni ama kuunga mkono jambo fulani au kulipinga. Matumizi ya nafsi ya kwanza na ya pili yanaonesha kuunga mkono jambo; wakati matumizi ya nafsi ya tatu yanaonesha kulipinga. Mapendekezo yanayotolea na utafiti huu ni kufanya utafiti mwingine katika kumbo mahususi za fasihi ili kuona namna ualbino kwa umahususi na ulemavu kwa ujumla unavyoumbwa katika kumbo hizo. Vilevile utafiti unapendekeza Nadharia ya Naratolojia itumiwe zaidi na wachambuzi wa kazi za kifasihi kwa kuwa inamwezesha mchambuzi kuufahamu uhalisia wa simulizi kupitia nafsi mahususi zinazotumika katika kusimulia. Nadharia hii iko karibu na uhalisia.

About Library

The University of Dar es Salaam Library is a vital source of scholarly information that facilitates users to get access to learning and research resources during their studies. It provides access to a wide range of resources in both print and digital formats and conducive reading environment for users, regardless of their physical conditions. All registered users are eligible to access library resources and can borrow print materials from general shelves for a specific period of time.

Useful Links

Koha Staff Login

University Research Repository

WebMail

Aris

Book Study Room

Mara Oral History

Hansard

SOCIAL MEDIA

Instagram

Facebook

Twitter

YouTube

WhatsApp

Ask Librarian

Contact Us

Postal Address
P.O.Box 35092
Dar es Salaam

Call Us: +255 22 2410500/9 Ext. 2165 ; Direct line +255 22 2410241

Fax No:: +255 22 2410241

Email:: directorlibrary@udsm.ac.tz

2025 University of Dar es Salaam - University Of Dar Es Salaam Library
Term of use / Privacy Policy